ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, February 20, 2018

DED MNASI AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA UJENZI WA MADARA YA SHULE ZA MSINGI ZA WILAYA YA ILEJE

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya Ileje Haji Mnasi akifanya kazi kwa vitendo alivyokuwa anafanya ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Izuba na shule ya msingi Ilulu na kuhakikisha wananchi wanachangia nguvu zao kuleta maendeleo kwenye vijiji vyao” alisema Mnasi
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya Ileje Haji Mnasi akifanya kazi kwa vitendo alivyokuwa anafanya ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Izuba na shule ya msingi Ilulu.
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya Ileje Haji Mnasi akibadilisha mawazo na baadhi ya viongozi walikuwa kwenye eneo la ujenzi wa  madarasa katika shule ya msingi Izuba na shule ya msingi Ilulu.

Na Fredy Mgunda,Ileje

HALMASHAURI ya wilaya ya Ileje mkoani songwe imetumia zaidi ya shilingi milioni mia moja themanini katika  ujenzi wa madarasa kwa kutumia fedha za EPFR ambazo hutolewa na serikali kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu kwa shule za msingi.
 
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kukagua miradi hiyo,mkurugenzi wa Ileje Haji Mnasi alisema kuwa jukumu la uongozi ni kuhakikisha kuwa pesa inayotolewa na serikali inatumika kama ilivyokusudiwa na serikali kuu kwa faida ya sekta ya elimu.

“Serikali inatoa pesa nyingi sana hivyo tusipo simamia vizuri pesa hizi zitapotea kitu ambacho Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Maguli hataki kabisa kusikia kuna pesa ambayo haitumiki kama ilivyokusudiwa ndio maana nimeamua kuanza kukagua miradi yote ambayo inatekelezwa katika halmashauri yetu” alisema Mnasi 

Mnasi aliwaomba wananchi kuchangia nguvu zao kuhakikisha shughuli za ujenzi wa madarasa na vituo vya afya wanajitolea vilivyo ili kuendelea kufanya kazi sambamba na kasi ya serikali ya awamu ya tano.

“Mimi binafsi nawaomba wananchi wajitolee kufyatua tofali ,kuchota maji,kubeba mchanga na kusomba tofali ambazo zinakuwa zimenunuliwa na serikali kwa ajili ya ujenzi ambao utakuwa na faida kwao na vizazi vijavyo” alisema Mnasi

Aidha Mnasi aliwapongeza wananchi wa halmashuri ya Ileje kwa kuendelea kujitolea kufanya kazi kwa kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali ya wamu ya tano ambayo imelenga kuleta maendeleo kwa wananchi wake

“Mpaka sasa kuna asilimia kubwa ambayo wananchi wamekuwa wakijitolea kufanya kazi za kimaendeleo ambazo zinawahusu japo sio kwa asilimia kubwa kutokana na idadi kubwa ya wananchi wanaoishi katika wialya hii hivyo nitoe wito kwa wananchi kuendelea kujitokeza kwenye maendeleo ili kuijenga ileje yetu mpya” alisema Mnasi

Mnasi alisema kuwa kipaumbele cha halmashauri kwa sasa ni kuhakikisha kuwa wanaboresha sekta ya elimu na sekta ya afya ili kukuza maendeleo ya wilaya kwa kasi kubwa.

“Ujenzi unaendelea ni wa madarasa ya shule ya msingi Izuba na shule ya msingi Ilulu na kuhakikisha wananchi wanachangia nguvu zao kuleta maendeleo kwenye vijiji vyao” alisema Mnasi

Naomba nimalizie kwa kupongeza serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Maguli kwa kufanya kazi kubwa ya kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo kwa kuboresha sekta za elimu,miundombinu afya na n.k

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.