ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 19, 2018

UGONJWA WA KIPINDUPINDU WAZIDI KUSHIKA KASI RUKWA.

Ugonjwa  wa kipindupindu ulioibuka mwezi Novemba mwaka jana katika tarafa ya Mtowisa wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa, umeendelea kushika kasi baada ya wagonjwa kuongezeka kutoka 170 wiki iliyopita na kufikia 207 katika kipindi cha siku tano.

Hayo yamebainika katika ziara ya mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Leonard Wangabo katika maeneo yaliyoathirika na ugonjwa wa kipindupindu na kubaini kuwa baadhi ya wavuvi walioondolewa katika kambi za uvuvi zilizofungwa wamekaidi na kurejea katika kambi hizo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga na Diwani wa kata ya Nankanga wamewashauri wananchi kuacha kukaidi maelekezo ya serikali ili kutokomeza ugonjwa wa kipindu pindu

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.