ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 2, 2017

BARCELONA: LIVERPOOL ILIHITAJI £183m KUMUUZA COUTINHO.

Barcelona imesema kuwa liverpool iliitisha £183m kwa uhamisho wa nyota wake Phillipe Countinho katika siku ya mwisho ya kukamilika kwa dirisha la uhamisho siku ya Ijumaa.

Liverpool wamekataa maombi matatu kutoka kwa mabingwa hao wa Uhispania kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 ambaye alikuwa ameomba uhamisho.

''Liverpool ilikuwa inataka Yuro milioni 200 na kwa kweli hatungeweza kukubali hilo'', alisema mkurugenzi wa Barcelona Albert Soler.

Tunamshukuru mchezaji huyo kwa juhudi alizofanya , kwa sababu alijaribu sana na kutuonyesha kuwa alitaka kuichezea Barcelona.

Soler ambaye alikuwa akizungumza katika mkutano na wanahabari siku ya Jumamosi aliongezea: Hali ilimalizika ilivyomalizika na hakuna chengine tunachoweza kufanya.
Barcelona ilimtaka Coutinho baada ya kumuuza Neymar kwa PSG kwa kitita kilichovunja rekodi ya uhamisho cha £200m.

Liverpool imesema kuwa Coutinho hauzwi na kukataa maombi ya £72m, £90m na jingine la £114m kabla ya kukamilika kwa dirisha la uhamisho nchini Uhispania ambalo lilifungwa siku moja baada ya lile la Uingereza kufungwa.

Coutinho aliyefunga mabao 14 msimu uliopita na kuhudumia miezi sita akiwa na jeraha la kifundo cha mguu aliweka kandarasi mpya ya miaka katika uwanja wa Anfield mnamo mwezi Januari.

Licha ya klabu za Ligi ya Premia kutumia £1.4bn kipindi chote cha kuhama wachezaji- ambayo ni rekodi mpya - Alexis Sanchez, Virgil van Dijk, Riyad Mahrez, Thomas Lemar, Diego Costa na Ross Barkley bado hawakufanikiwa kuhama.

Siku ya mwisho ya kuhama wachezaji msimu uliopita ilikuwa £155m.
Chelsea walitumia £35m kumnunua Danny Drinkwater naye Mamadou Sakho akanunuliwa £26m na Crystal Palace kutoka Liverpool, taarifa za kuhama kwao zikitangazwa baada ya muda rasmi wa kuhama wachezaji.

Wawili hao ndio waliosaidia kuvunja rekodi ya mwaka jana.

Chelsea walinunua pia Davide Zappacosta, Spurs wakamchukua mshambuliaji wa Swansea Fernando Llorente kwa £15m, klabu hiyo ya Wales nayo ikajaza nafasi hiyo kwa kumchukua Wilfried Bony kwa £12m.

WANAFUNZI 7 WAFARIKI KATIKA MOTO ULIOCHOMA BWENI KENYA.

Maafisa wa polisi wakishika doria nje ya shule ya Moi Girls liliopo jijini Nairobi nchini Kenya Wanafunzi saba wamefariki na makumi wengine wakijeruhiwa baada ya moto kuchoma bweni la shule ya Moi Girls mjini Nairobi.

Waziri wa elimu Fred Matiang'i amesema kuwa wanafunzi wengine 10 walijeruhiwa na wamelazwa hospitalini.

Wawili kati ya 10 wako katika hali mbaya ,kulingana na madaktari huku wengine wanane wakiwa hawako katika hali mbaya.

Parents and some students at Moi Girls School

Wazazi na baadhi ya watoto wa shule ya Moi Girls mjini Nairobi wakifarijiana kwenye eneo la tukio.
 
Takriban wanafunzi 10 wamerodheshwa kuwa hawajulikani waliko kulingana na kitengo cha habari cha maafisa wa msalaba mwekundu katika shule hiyo.


Kenya Red Cross personnel attend to a woman who
Wafanyakazi wa chama cha msalaba mwekundu wakimsaidia mama aliyezimia mara baa ya tukio la kufariki watoto shule ya Moi Girls mjini Nairobi. 
 
Matiang'i amesema kuwa shule hiyo imefungwa kwa wiki mbili huku uchunguzi ukianzishwa kuhusiana na sababu ya moto huo.

Waziri huyo hatahivyo amesema kuwa wanafunzi wa kidato cha nne wataendelea na masomo yao ifikiapo siku ya Ijumaa na watasaidiwa kuendelea na masomo yao wakati ambapo wanajianda kufanya mtihani wa kidato cha nne wa KCSE.

Amesema kuwa kundi la wataalam wa upasuaji ikiwemo madaktari wako katika shule hiyo kubaini chanzo cha moto huo.

Amesema kuwa mkuu wa shule hiyo amewataka wazazi kuwachukua wanawao.

Relatives of students at Moi Girls School
Ndugu jamaa  wa wanafunzi wa Moi Girls School Nairobi wakitokwa na machozi baada ya kufariki kwa wanafunzi hao 7 huku wengine 10 wakiwa majeruhi.
 
Bwana Matiang'i aliandamana na gavana wa Nairobi Mike Sonko.

Kulingana na gazeti la Daily Nation nchini humo mwanafunzi mmoja wa kidato cha kwanza ambaye alikuwa miongoni mwa wale waliotibiwa baada ya kisa hicho alisema kuwa moto huo ulianza mwendo wa saa saba usiku.

Alisema kuwa bweni lililochomeka lilikuwa na wanafunzi wa kidato cha kwanza na kwamba kulikuwa na makelele ya wanafunzi waliojaribu kujinusuru mbalii na mkanyagano huku wasichana wakijaribu kutoka ndani ya bweni hilo.

HII YA KENYA NI BALAA, AJIRA ZA TRA ZAONYESHA UKUBWA WA TATIZO LA AJIRA, MTOTO AJERUHIWA PAJANI AKIPAMBANA NA SIMBA



Hii ya Kenya ni balaa, Ajira za TRA zaonyesha ukubwa wa tatizo la ajira, Mtoto ajeruhiwa pajani akipambana na Simba.
 
Hoja 2 kuivusha Kenya uchaguzi wa marudio, Mufti Zuberi awashukia waliwatapeli Mahujaji, TFF yaamua kumlinda Tshishimbi asizinguliwe. Habarika na dondoo hizi hapa.

WANANCHI WAVAMIWA NA CHUI NA KUJERUHIWA VIBAYA JIMBO LA ILEMELA MWANZA

 Tunachukua fursa hii kutoa pole kwa naibu waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi na mbunge wa Ilemela mhe Angelina Mabula kwa wananchi wake sita kuvamiwa na kujeruhiwa na Chui jana eneo la Kabangaja kata ya bugogwa jimboni Ilemela.



Friday, September 1, 2017

MAFURIKO NIGERIA YAPELEKEA WATU 110,000 KUPOTEZA MAKAZI.

Mafuriko Nigeria yapelekea watu 110,000 kupoteza makazi
Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria amesema watu zaidi ya laki moja na elfu kumi wamepoteza makazi yao baada ya kutokea mafuruko katika jimbo la Benue katikati mwa nchi hiyo.
Katika taarifa ya siku ya Ijumaa kupitia akaunti yake ya Twitter, Rais Buhari amesema timu za uokoaji zimefika katika eneo la maafa kusaidia familia za waathirika.
Hadi hivi sasa hakuna taarifa kamili kuhusu hasara iliyopatikana kufuatia mafuriko hayo.
Tokea mwanzoni mwa mwaka huu, Nigeria imekumbwa na mvua kali za msimu ambazo zimesababisha hasara katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi.
Rais Buhari wa Nigeria.
Jimbo la Benue linategemea sana kilimo na hukumbwa na mafuriko mara kwa mara kutokana na mvua kali na kufunguliwa mabwawa ya nchi jirani ya Cameroon. Mwaka 2012 Nigeria ilikumbwa na mafuruko mabaya katika majimbo 30 kati ya 36 ya nchi hiyo. Mamia ya watu waliaga dunia na wengine milioni mbili kuachwa bila makazi.

MAHAKAMA YA JUU KENYA YATENGUA MATOKEO YA UCHAGUZI WA RAIS.

Mahakama ya Juu Kenya yatengua matokeo ya uchaguzi wa Rais
Mahakama ya Juu ya Kenya imetengua matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi uliopita nchini humo na kumpa ushindi Rais wa sasa wa nchi hiyo, Uhuru Kenyatta.
Mahakama ya Juu ya Kenya imetengua matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi uliopita nchini humo na kumpa ushindi Rais wa sasa wa nchi hiyo, Uhuru Kenyatta huku kinara wa muungano wa upinzani wa NASA Raila Odinga akiibuka wa pili.

Jopo la majaji sita, na kwa uamuzi wa wengi, leo Ijumaa limesema iligundua kuwa Tume ya Uchaguzi haikuweza kuendesha zoezi la uchaguzi kulingana na Katiba na Sheria Uchaguzi.
"Baada ya kuzingatia ushahidi wote, tumeridhika kuwa uchaguzi haukufanyika kwa mujibu wa kanuni za Katiba na kanuni husika", amesema Jaji Mkuu wa Kenya David Maraga.
Majaji wawili katika jopo hilo walipinga uamuzi wa kubatilisha uchaguzi. Uchaguzi mpya wa Rais wa Kenya utafanyika siku sitini zijazo.

Baada ya Mahakama ya Juu Zaidi kufutilia mbali ushindi wa Uhuru Kenyatta katika uchaguzi wa urais uliofanyika Agosti 8, Uhuru na chama amesisitiza kutoridhishwa na uamuzi huo. Akiongea kutoka Ikulu ya rais, Uhuru alipinga uamuzi huo japo atauheshimu huku akisisitiza kuwa yuko tayari kwa ajili ya marudio ya uchaguzi.

Kinara wa upinzani Kenya Raila Odinga akisherehekea ushindi mahakamani.
Wakati huo huo, wakizungumza nje ya Mahakama ya Juu zaidi baada ya kushinda kesi hiyo, viongozi hao walisema, makamishna wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) waliosababisha mchakato wa uchaguzi mbovu, ni lazima kufunguliwa mashtaka.
 
Wakiongozwa na Raila Odinga, viongozi hao walisema, hawataruhusu makamishna hao kusimamia uchaguzi tena unaotarajiwa katika kipindi cha miezi miwili.

Shughuli katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi zilikwama kwa muda baada ya wafuasi wa NASA kuingia jijini kwa mbwembwe wakishereheka ushindi wao kwenye kesi dhidi ya ushindi wa Uhuru Kenyatta. Katika upande wa pili wafuasi wa Rais Kenyatta na chama cha Jubilee walionekana kutulia huku wakisema watajitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa marudio ili kuhakikisha wanapata ushindi.

Thursday, August 31, 2017

MANGULA AKUTANA NA NAIBU WAZIRI WA CPC.

 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philipo Mangua akimkaribisha Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, Agosti 31, 2017. Katikati ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole. (Picha na Bashir Nkoromo).

Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philipo Mangua (kulia) akiongoza mazungumzo  baina yake na Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping (kulia) katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, Agosti 31, 2017. (Picha na Bashir Nkoromo).

 Naibu Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Ujenzi ya IDCPC Kanda ya Afrika,  Wang Heming
akipiga picha mandhari ya eneo kitakakojenjwa Chuo Kikuu cha Viongozi wa Siasa cha Mwalimu Nyerere, Kibaha mkoa wa Pwani, alipotembelea eneo hilo,  Agosti 30, 2017. Kushoto ni Katibu waNEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ngemela Lubinza.(Picha na Bashir Nkoromo).

MAMIA WAMIMINIKA KUJISAJILI KATIKA MFUKO WA FIDIA (WCF) IKIWA UTEKELEZAJI WA AGIZO LA WAZIRI JENISTA MHAGAMA

Meneja Matekelezo  Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, WCF, Bw.Victor Luvena, (kulia), akiwahudumia waajiri waliofika kujisajili na kulipa michango leo Agosti 31, 2017.

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
MUITIKIO wa waajiri kujisajili na kulipa michango katika Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi (WCF) umekuwa wa kuridhisha hususani Mwezi Agosti, Meneja Matekelezo Bw. Victor Luvena amesema leo Agosti 31, 2017.
Itakumbukwa ya kwamba, tarehe 23 Julai 2017 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama (Mb), alitoa siku 30 kwa waajiri wote nchini ambao walikuwa hawajasajili kuhakikisha wanajisajili katika Mfuko na wanawasilisha michango kwa wakati, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao na kama Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi inavyoelekeza.
“Kwakweli tunamshukuru Mheshimiwa Waziri kwa agizo alilolitoa kwani limetoa msukumo mkubwa, waajiri wengi wamejitokeza kutekeleza wajibu wao wa kisheria wa kujisajili na kuwasilisha michango katika Mfuko.” Alisema Bw. Luvena
K-VIS Blog ilishuhudia idadi kubwa ya waajiri wakiwa wamejitokeza leo Agosti 31, 2017 ambayo ndiyo siku ya mwisho kwa waajiri kutekeleza agizo la Mheshimiwa waziri, wakiwa wamejazana kwenye ofisi za WCF  kujisajili na kuwasilisha michango, ambapo kazi hiyo ya kuwahudumia ilikuwa ikiongozwa na Meneja Matekelezo - WCF, Bw.Victor Ruvena.
 Waajiri, wakihudumiwa na maafisa wa WCF, leo Agosti 31, 2017.

 Afisa Matekelezo wa WCF, Bi. Gladness Madembwe, (kulia), akimkabidhi cheti cha usajili Bw.Sultani Ali kutoka kampuni ya Marifas Refregerator ya jijini Dar es Salaam.
 Afisa Matekelezo wa WCF, Bw.Edward Kerenge, (kushoto), akiwahudumia waajiri waliofika kujisajili na Mfuko leo Agosti 31, 2017.
  Afisa Matekelezo wa WCF, Bw.Edward Kerenge, (kulia), akiwahudumia waajiri waliofika kujisajili na Mfuko leo Agosti 31, 2017.
 Afisa Matekelezo Msaidizi wa WCF, Bi.Emiliana J.Gwagilo, akimsikiliza Mwajiri huyu aliyefika kupatiwa huduma leo Agosti 31, 2017.
  Afisa Matekelezo Msaidizi wa WCF, Bi.Emiliana J.Gwagilo, (kushoto), akimuhudumia Mwajiri huyu aliyefika kupatiwa huduma leo Agosti 31, 2017.
  Afisa Matekelezo wa WCF, Bi. Gladness Madembwe,(kushoto), akimuhudumia Bw. Sultani Ali kutoka kampuni ya Marifas Refrigeration, ya jijini Dar es Salaam.
 Meneja Matekelezo  Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, WCF, Bw.Victor Luvena, (kulia), akiwasikiliza waajiri waliofika leo Agosti 31, 2017 ili kupatiwa huduma ya usajili na uwasilishaji michango katika Mfuko huo.
 Maafisa wa WCF (kulia), wakimsikiliza Mama huyu mwajiri aliyefika kupatiwa huduma.



KUELEKEA SIKUKUU YA EID EL HADJI JESHI LA POLISI DAR ES SALAAM LIMEKUJA NA TAARIFA HII.

Kesho ni siku kuu ya Eid el Hadji, Kamanda wa Polisi wa Kanda maalumu ya Dar es salam SACP Lazaro Mambosasa amepiga marufuku shughuli aina ya Disco toto katika Jiji la Dar es salaam.

Akizungumza leo Jijini humo na vyombo vya habari ameeleza kuwa hatua hiyo imefuta kwakuwa mpaka sasa hawajapokea maombi kutoka kwa wamiliki wa kumbi za starehe kwaajili ya Watoto kwahiyo jeshi la polisi haliwezi kuruhusu bila kujiridhisha kama kumbi hizo zina hewa ya kutosha.
"Nitoe rai kwa wananchi katika sikukuu hii ambayo huitwa sikukuu ya kuchinja, tunawaomba wananchi washerehekee pamoja na familia zao lakini uangaliazi kwa watoto uwe ni wa hali ya juu, wasiwaache watoto wadogo kuingia kwenye kumbi za starehe au kwenda maeneo mengine ambayo kimsingi ni hatarishi kwa watoto hao" BOFYA PLAY KUMSIKIA

Hata hivyo Mambosasa amewahakikishia Wakaazi wote wa Jiji la Dar es es salaam kuwa wamejipanga vyema kuhakikisha sikukuu hiyo inamalizika kwa amani utulivu

Sambamba hilo amewataka Wana Dar es salaam kushirikiana na jeshi hilo ili kufichua vitendo vya kihalifu.

MWIGULU AFUNGUA KIKAO CHA KUJADILI UREJESHAJI WA WAKIMBIZI WA BURUNDI WALIO TAYARI KUREJEA NCHINI KWAO



 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba, akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kikao cha 19 kinachoshirikisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani(UNHCR),lengo ni kujadili na kuwekeana makubaliano juu ya Mpango wa Kuwarejesha Wakimbizi wa Burundi wanaohifadhiwa katika makambi ya wakimbizi ambao wako tayari kurejea nchini kwao.Kikao hicho kimefanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere,jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani na Elimu ya Uzalendo kutoka nchini Burundi,Pascal Barandagiye, akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kikao cha 19 kinachoshirikisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani(UNHCR),lengo ni kujadili na kuwekeana makubaliano juu ya Mpango wa Kuwarejesha Wakimbizi wa Burundi wanaohifadhiwa katika makambi ya wakimbizi, ambao wako tayari kurejea nchini kwao.Kikao hicho kimefanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere,jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mwakilishi wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi  Duniani (UNHCR) nchini Tanzania,Chansa Kapaya, akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kikao cha 19 kinachoshirikisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani(UNHCR),lengo ni kujadili na kuwekeana makubaliano juu ya Mpango wa Kuwarejesha Wakimbizi wa Burundi wanaohifadhiwa katika makambi ya wakimbizi ambao wako tayari kurejea nchini kwao.Kikao hicho kimefanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere,jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba, akipitia nyaraka mbalimbali wakatiKikao cha 19 kinachoshirikisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani(UNHCR),lengo ni kujadili na kuwekeana makubaliano juu ya Mpango wa Kuwarejesha Wakimbizi wa Burundi wanaohifadhiwa katika makambi ya wakimbizi ambao wako tayari kurejea nchini kwao.Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi,Harrison mseke.Kikao hicho kimefanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere,jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba(watano kulia), Waziri wa Mambo ya Ndani na Elimu ya Uzalendo kutoka nchini Burundi,Pascal Barandagiye,(wasita kulia), na Mwakilishi wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi  Duniani (UNHCR) nchini Tanzania,Chansa Kapaya(wanne kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Kikao cha 19 kinachoshirikisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani(UNHCR),lengo ni kujadili na kuwekeana makubaliano juu ya Mpango wa Kuwarejesha Wakimbizi wa Burundi wanaohifadhiwa katika makambi ya wakimbizi ambao wako tayari kurejea nchini kwao.Kikao hicho kimefanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere,jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.

POLISI MWANZA YAPIGA STOP MABASI MABOVU 22.



NA ZEPHANIA MANDIA WA G.SENGOBLOG

Zaidi ya abiria mia tano waliokuwa wakitarajia kusafiri kwenda mikoa mbalimbali ya ndani na nje ya nchi, leo wamejikuta wakikabiliwa na adha ya usafiri, baada ya Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza kupitia kikosi cha usalama barabarani, kuzuia mabasi 22 kati ya 79 yaliyokaguliwa kutoendelea na safari kutokana na ubovu.

Jeshi hilo limelazimika kuendesha Oparesheni hiyo ya kustukiza katika vituo vikuu vya mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi vya Buzuruga na Nyegezi, baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa abiria kuwa baadhi ya mabasi, yamekuwa yakikwamisha safari zao na kuwalaza barabarani kutokana na ubovu.

Kutokana na Oparesheni hiyo mabasi 57 kati ya sabini na tisa yametozwa faini, baada ya kubainika kuwa na makosa mbalimbali, huku ishirini na mbili yakizuiwa kabisa kutoendelea kutoa huduma kutokana na ubovu, hatua ambayo inalenga pia kupunguza ajali za barabarani zitokana na ubovu wa Magari.   

Kamanda wa polisi mkoa wa Ahmed Msangi, amesema kuwa zoezi la ukaguzi wa mabasi yaendayo mikoani litakuwa endelevu, ili kudhibiti mianya ya madereva wanaokiuka sheria za usalama barabarani kwa kuendesha mabasi mabovu, yanayochangia kuwepo na ajali za barabarani.