ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 15, 2017

MWANASHERIA WA GGM MBARONI KWA KUMNYIMA NYARAKA NAIBU WAZIRI

Mwanasheria Mkuu wa Mgodi wa dhahabu wa Geita(GGM) David Nzarigo akipandishwa kwenye gari ya Polisi Baada ya agizo la  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh,Kangi Lugola.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh,Kangi Lugola akipokea taarifa ya shughuli zinazofanywa na Mgodi huo.

Mganga Mkuu wa Mgodi ambaye pia anasimamia kitengo cha mazingira Mgodini wa Dhahabu wa Geita(GGM)akitoa taarifa ya namna ambavyo mgodi umekuwa ukihifadhi mazingira.

Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akitazama baadhi ya nyaraka wakati ambapo Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh,Kangi Lugola.

Mwanasheria Mkuu wa Mgodi wa dhahabu wa Geita(GGM) David Nzarigo akipelekwa kwenye gari la polisi na askali baada ya agizo la Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh,Kangi Lugola.

Moja kati ya Nyumba ambayo hipo ndani ya eneo la Mgodi.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh,Kangi Lugola akikagua madarasa ambayo yanaonekana kuharibiwa na mipasuko.


 Na Joel Maduka,Geita
Mwanasheria Mkuu wa Mgodi wa dhahabu wa Geita(GGM) David Nzarigo amekamatwa na serikali baada ya kukutwa na nyaraka za serikali .
                                                                                                                                   
Mwanasheria huyo amekamatwa kwa  amri ya Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh,Kangi Lugola alipotembelea Mgodi huo ambapo pamoja na mambo mengine amebaini mgodi huo kuwa unaendesha shughuli zake bila kufuata sheria ya mazingira .

Mhe. Lugola akiwa katika ziara ya kikazi ya siku mbili  Wilayani Geita ameagiza kukamatwa kwa mwanasheria  Mkuu  wa Mgodi wa dhahabu wa  Geita (GGM) David Nzogila baada ya kukutwa na nyaraka za serikali ambazo hazijawa rasmi kutumika kutoka taasisi  ya wakala wa utafiti wa jiolojia Tanzania(GST).

 Hata hivyo katika hali hisiyo ya kawaida na  bila kutarajia mwanasheria huyo aliyekuwa akiukingia kifua mgodi huo  ili usikumbane na rungu la fidia ya uharibifu wa kimazingira kama sheria inavyotamka alijikuta akimweleza Naibu Waziri kuwa anayo ripoti ya GST aliyodai haijaeleza iwapo mgodi huo unahusika moja kwa moja kwenye uharibifu hivyo mgodi huo usibebeshwe mzigo huo.

Kutokana na hali hiyo,Naibu Waziri Lugola aliomba apatiwe riporti hiyo ili ajiridhishe lakini mwanasheria huyo akijibu kwa kujiamnini alimtaka kiongozi huyo wa juu   kutumia mbinu zake kuipata Serikalini lakini yeye  hawezi kutoa nyaraka ya serikali, jambo  lililomkasirisha Naibu Waziri  wa Muungano na Mazingira na kutoa agizo la kukamatwa mara moja.

Diwani wa kata ya mtakuja Constatine Morandi ameelezea kuwa wananchi wamekuwa wakisumbuliwa muda mrefu na mgodi bila ya kupatiwa fidia  na kwamba kutokana na wao kuwa ndani ya bikoni kumesababisha kutokupatiwa huduma mbali mbali za kijamii  hivyo ni vyema kwa serikali wakaweka nguvu kuwasaidia wananchi hao.

Bw Abdallah Omary-Mkazi Nyamalembo alimweleza Naibu waziri  kwamba wamekuwa wakiishi maisha ya mashaka kutokana na hali ilivyo ya maeneo hayo ya mgodini na kwamba mgodi ulikwisha wai kuwapatia fidia ya shilingi elfu ishirini jambo ambalo limeonekana kuwa ni udhalilishaji kwani pesa hiyo ni ndogo.


 Kwa upande wake Makamu wa Rais wa mgodi huo Saimon Shayo,alisema kuwa  eneo ambalo wananchi wamekuwa wakilalamika kuhusu suala la fidia hadi sasa kuna nyumba mbili na kwamba fidia ya kwanza walilipa kiasi cha sh,Bilion Moja na waliipatia serikali iweze kuwafidia wananchi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.