ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 16, 2017

MUGABE ANG'ANG'ANIA MADARAKA, AU NA UN ZATOA KAULI.

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ambaye yuko katika ncha ya kuuzuliwa amekataa kuachia madaraka akisisitiza kuwa yeye ndiye kiongozi halali wa nchi hiyo.

Duru za habari zimeliambia shirika la habari la Reuters kuwa, Mugabe amekataa upatanishi wa Askofu wa Kanisa Katoliki nchini humo Fidelis Mukonori, ambaye alikuwa anaongoza mazungumzo kati ya rais huyo mkongwe mwenye umri wa miaka 93 na makamanda wa jeshi la nchi hiyo.

Jeshi hilo jana lilitangaza kuwa Mugabe na familia yake wako kwenye kizuizi cha nyumbani na kuongeza kuwa litawapandisha kizimbani wale liliowataja kama "wahalifu" waliomzunguka kiongozi huyo ambao wameisababishia nchi hiyo madhara na hasara za kiuchumi na kijamii.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.