ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, October 20, 2017

MISUNGWI WAFUNGUKA JINSI HONGO INAVYOTUMIKA KUFICHA WAHALIFU WA UBAKAJI NA UKATILI



Jeshi la polisi mkoani Mwanza kupitia mtandao wa Polisi Wanawake TPF NET mkoani hapa limewataka wanawake kuvunja ukimya na kutoa taarifa mbalimbali za uhalifu na wahalifu ikiwemo vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto.

Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi Wanawake mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Afisa Mnadhimu wa jeshi hilo Kamishna wa Polisi Advera Bulimba wakati alipotembelea wilaya ya Misungwi na kuzungumza na wanawake kwa lengo la kutoa elimu ya Kuzzuia na kupambana na uhalifu kwa jamii ya wakazi wa wilaya hiyo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.