ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 8, 2017

MAGHOROFA YA LUGUMI KUPIGWA MNADA KESHO.

Kampuni ya Udalali ya Yono kesho itapiga mnada maghorofa yanayomilikiwa na kampuni ya Lugumi.

Maghorofa hayo mawili ambayo yapo sehemu tofauti moja likiwa mtaa wa Mazengo Upanga na lingine likiwa Mbweni jijini Dar es Salaam..

Mkurugenzi wa Yono, Scolastica Kevela amesema leo Ijumaa kuwa wametumia njia mbalimbali ili kufanikisha mnada huo kufanyika hasa kwa kutumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Amesema hawezi kutaja gharama halisi ya mali hizo na deni ambalo kampuni hiyo inadaiwa na Mamlaka ya Mapato(TRA) hivyo hao ndio wanaoweza kutoa majibu hayo.

"Kazi yetu sisi ni kupiga mnada tu, gharama ya deni na thamani ya mali hizo TRA ndio wanatakiwa kutolea majibu,"amesema Kevela.

Amesema fedha watakazozipata zitakwenda kusaidia nchi katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.