ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 29, 2017

JAFO: WATENDAJI MSILETE LELEMAMA USIMAMIZI MIRADI YA MAENDELEO

 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua Kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni, Wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu na Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki (CCM) Mhe Daniel Mtuka
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu wakikagua chumba cha kuhifadhia maiti katika kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akitembelea na kukagua mradi wa maji Kintinku/Lusilile wilayani Manyoni
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akimshukuru Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo kwa ukaguzi wa miradi ya maendeleo.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua mradi wa maji Kintinku/Lusilile wilayani Manyoni
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua chumba cha dawa katika Kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni, Mwingine ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu
  
Na Mathias Canal, Singida

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Tamisemi) Mhe Seleman S. Jaffo (Mb) amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida kuanza haraka Mradi wa Ujenzi wa Chumba Cha upasuaji, na Ujenzi wa wodi ya kisasa.

Naibu Waziri Jaffo ametoa maagizo hayo wakati alipokuwa akizungumza na watumishi wa kituo Cha afya Kintinku mara Baada ya kutembele na kujionea uduni wa upatikanaji wa Huduma katika kituo hicho.

Alisema Mradi huo utaambatana na Ujenzi wa maabara kwa ajili ya vipimo kwa wagonjwa, Ujenzi wa eneo la kuchomea taka na Ukarabati wa eneo la kuhifadhia maiti.

Jafo ameonyesha kukerwa na ucheleweshwaji wa kuanza Ujenzi huo licha ya serikali kupeleka fedha kiasi cha shilingi milioni 500 katika mwaka wa fedha 2017/2018 zitakazotosha kukamilisha Ujenzi wote.

Alisema katika awamu ya Pili zitatolewa fedha kiasi cha shilingi milioni 220 zitakazotumika kununua vifaa vyote katika Chumba Cha upasuaji na vifaa tiba kwa ujumla.

Naibu Waziri Jafo alisema kitendo Cha kuchelewa kuanza Ujenzi huo kinachelewesha kuwapatia huduma bora wananchi ambayo inahubiriwa na serikali ya awamu tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli.

"Haiwezekani Rais anatoa fedha kwa ajili ya kuboresha sekta mbalimbali nchini ikiwemo sekta ya Afya halafu kuna watu wachache wanashindwa kusimama vizuri fedha Hizo Jambo ambalo linapelekea serikali kulaumiwa na wananchi" Alisema Jaffo

Katika hatua nyingine Mhe Jaffo alimuagiza mhandisi wa Maji Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Vijijini Eng Gasto Mbondo kutekeleza mpango wa shughuli za utoaji wa Huduma ya maji kupitia Mradi wa kisima Cha Kintinku/Lusilile kilichopo Kijiji Cha Mbwasa (Mbwasa Well Field) kwani eneo Hilo linaonekana kuwa na maji ya kutosha.

Akikagua mradi huo Mhe Jaffo alisema tatizo kubwa kwa wananchi Ni pamoja na changamoto sugu ya upatikanaji Huduma za maji hususani vijijini na kukamilika kwa mradi huo utapunguza umbali na muda wanaotumia wananchi kutafuta maji. 

Awali Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Eng Gasto Mbondo akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za utoaji wa Huduma ya maji alisema kuwa Mradi huo wa maji wa Kintinku/Lusilile utakapokamilika unatarajia kuhudumia watu wapatao 45,417 kwa kuongeza 19.2% kutoka 42.1% iliyopo mpaka 61.3% na utakuwa na Vituo 81 vya kuchotea maji (DPs).

Naye Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Alisema kuwa utekelezaji wa miradi hiyo utasimamiwa kwa karibu na ofisi yake ili kuongeza Hamasa na tija.

Pia alisema katika Mradi wa Ujenzi wa majengo kwa ajili ya kituo Cha Afya Kintinku asilimia kubwa ya mafundi watatoka katika Wilaya ya Manyoni ili kutoa ajira kwa wananchi husika.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.