ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, July 27, 2017

BIASHARA HARAMU YA USAFIRISHAJI BINADAMU

Katibu wa Kamati ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu,Seperatus Fella, akizungumza kwenye mkutano uliowakutanisha  wajumbe wa Kamati na Sekretarieti ya Kitaifa ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu,lengo ikiwa ni kupitia Sheria mbalimbali zinazosimamia biashara hiyo.Wengine ni Mwenyekiti wa kamati hiyo () na Mkurugenzi Mradi wa kuzuia biashara hiyo kutoka Taasisi ya Kimataifa ya RTI,Dk. Lyungai Mbilinyi.Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi,jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi Mradi wa Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu kutoka Taasisi ya Kimataifa ya RTI,Dk. Lyungai Mbilinyi,akizungumza kwenye mkutano uliowakutanisha  wajumbe wa Kamati na Sekretarieti ya Kitaifa ya Kuzuia na Kupambana na Biashara hiyo,lengo ikiwa ni kupitia Sheria mbalimbali zinazosimamia biashara hiyo.Wengine ni Mwenyekiti wa kamati hiyo () na Katibu wa Kamati ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu,Seperatus Fella.Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi,jijini Dar es Salaam
Mjumbe wa Kamati na Sekretarieti ya Kitaifa ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu,() akizungumza wakati wa mkutano wa  kupitia Sheria mbalimbali zinazosimamia biashara hiyo.Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi,jijini Dar es Salaam
Mjumbe wa Kamati na Sekretarieti ya Kitaifa ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu,() akizungumza wakati wa mkutano wa  kupitia Sheria mbalimbali zinazosimamia biashara hiyo.Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi,jijini Dar es Salaam
Nchi ya Tanzania imetajwa kuwa miongoni mwa mataifa yanayoshamiri kwa biashara haramu ya kusafirisha binadamu kwa ajili ya utumwa wa ngono duniani.

Kupitia taarifa iliyotolewa mnamo mwezi July 4 mwaka 2016 na Katibu wa Sekretarieti ya Kitaifa ya kuzuia na kupambana na biashara haramu ya bianadamu kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, Bw. Separatus Fella alipokuwa akiongea katika mkutano uliondaliwa na Shirika la Kimataifa la Msaada wa Sheria (NOLA) kwa lengo la kutoa elimu juu ya mdhara ya kusafirisha watoto.

NUKUU YAKE INASEMA "Tanzania ni mkondo na chanzo cha usafirishaji wa wanawake na watoto wanaopelekwa kwenye biashara ya utumwa wa ngono katika mataifa mengine, na hii ni kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa nchini Marekani," alisema Fella.

Aidha wasafirishaji binadamu wamekuwa wakitumia Tanzania kama chanzo cha kupitisha na kupata watoto wanawake wakufanya biashara hiyo.

Baadhi ya mambo yanayochochea biashara ya usafirishaji haramu binadamua ni pamoja na umasikini na kukata tamaa, ukatili wa majumbani, njaa na vita, ukosefu wa ajira na mishahara kidogo, ndoa kuvunjika, kukosekana kwa usawa wa kijinsia na ukosefu wa elimu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.