ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 29, 2017

MUUMINI MWINJUMA NI CHUMA CHA RELI AISHTUKIZA MWANZA KWA SHOW YA HATARI USIKU WA KUAMKIA LEO.

Mwanamuziki mkurugenzi wa Double M Plus Muumini Mwinjuma akiimba katika show yake iliyofanyika jana ijumaa ndani ya Villa Park Mwanza na kusisismua wengi waliohudhuria.
Kwa mara nyingine tena, Double M Plus tena kama mashambulizi ya kustukiza hivi usiku wa kuamkia leo yaani jana ijumaa wameangusha mbungi la burudani katika kiota cha Villa Park Mwanza.

Bosi wa bendi hiyo Mwinjuma Muumin akiwa na wakali wengine wa bendi hiyo amefunika tena sana kwa masauti yake matamu. 

Double M Plus ilitimua vumbi ndani ya ukumbi huo kwenye onyesho la kufungua pazia ya ratiba yao ya kutumbiza Kanda ya Ziwa wakiwapa likizo fupi ndugu zao Super Kamanyola.

Double M Plus ikadhihirisha kuwa ina utajiri wa program ya nyimbo pendwa (hit songs) kuanzia zile za Mchinga Sound, Tam Tam na Double M Sound ambako kote huko Muumin alishiriki kuzalisha kazi nyingi zilizotesa ndani na nje ya Bongo. 

Nyimbo kama “Kiu ya Mapenzi”, “Tunda”, “Mgumba”, “Kilio Cha Yatima”, “Kisiki Cha Mpingo” na nyingine nyingi zilinguruma Equator Grill na kusisimua mashabiki waliofika kwenye ukumbi huo ulioko Kirumba jijini Mwanza.














Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.