ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, July 10, 2017

MHE. HALIMA MDEE AACHIWA KWA DHAMANA.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu chini ya Hakimu Victoria Nongwa imemuachia Mbunge Halima Mdee kwa Dhamana ya ahadi ya Shilingi 10 pamoja na Wadhamini wake wawili, na atatakiwa  kurudi mahakamani tarehe 7,
Katika kesi namba 218 ya 2017, Kupitia Nasorro katuga Wakili wa Jamhuri, Halima Amesomewa shitaka la kutumia lugha ya matusi Dhidi ya Rais Magufuli "Rais anaongea Hovyo, Afungwe Breki" Hata hivyo alipoulizwa kama nikweli Mdee alikana shitaka hilo.

Mbunge wa Jimbo la Kawe Halima Mdee alifikishwa katika mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu Leo Jijini Dar es salaam majira ya Asubuhi.

 Halima Mdee (Chadema), alikamatwa Julai 4 Jioni, na Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni kwa na agizo la Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi. Kwa kile kilichodaiwa alitoa lugha ya kumtukana Rais Magufuli.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.