KIUNGO anayeweza kucheza nafasi zote za ulinzi, Erasto Edward Nyoni yuko
mbioni kujiunga na mabingwa wa Tanzania, Yanga baada ya kumaliza
mkataba wake Azam FC.
Nyoni yupo kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars
inayojiandaa kwa mchezo na Rwanda Jumamosi Uwanja wa CCM Kirumba mjini
Mwanza kuwania tiketi ya Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN),
michuano inayohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee –
na Yanga wanatarajia kumalizana naye kabisa baada ya mechi hiyo.
“Mazungumzo na Nyoni yamekwenda vizuri na wakati wowote tunaweza
kumalizana naye, pengine baada ya mechi tu dhidi ya Rwanda,”kimesema
chanzo kutoka Yanga.
Benchi la Ufundi la Yanga, chini ya Kocha Mkuu, Mzambia George
Lwandamina kwa kushirikiana na Sekretarieti chini ya Katibu Mkuu,
Charles Boniface Mkwasa ambaye kitaaluma ni kocha kwa pamoja
wamejiridhisha Nyoni ni mchezaji ambaye wanamuhitaji kikosini.
Na hiyo ni kwa sababu huyo ni ‘kiraka’ anayeweza kucheza nafasi yoyote
ya ulinzi kuanzia kiungo wa ulinzi – lakini uzoefu na weledi wake kisoka
ni vitu vingine vinavyomuunganisha na Yanga katika siku za mwishoni za
maisha yake ya uwanjani.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.