Gazeti la The Guardian linalochapishwa mjini
London, Uingereza limeandika kuwa, hatua za Rais Donald Trump wa
Marekani zinaisambaratisha nchi hiyo.
Mtandao wa habari wa gazeti hilo
sambamba na kuashiria kipindi cha miezi sita tu tangu aingie madarakani
rais huyo wa Marekani, limeandika kuwa, ahadi za kiuchumi na kibiashara
za Trump hazina mustakbali wowote wa kutekelezeka. Aidha limeandika kuwa
hadi sasa Trump hajaweza kutekeleza ahadi zake hizo kuhusiana na
kuufanyia mabadiliko mfumo wa fedha wa Marekani.
Gazeti hilo limezungumzia pia hatua ya
Marekani ya kujiondoka katika mkataba wa hali ya hewa wa mjini Paris,
Ufaransa na kuandika kuwa, katika kipindi cha chini ya miezi sita pekee,
Trump ametupilia mbali mipango muhimu ya mtangulizi wake, Barack Obama
hususan katika uga wa mazingira.
Pia limeitaja amri ya Rais Donald Trump dhidi ya uhajiri kuwa ni hatua ya tatu ya kuisambaratisha Marekani na kufafanua kuwa, amri hiyo inayowazuia raia wa mataifa sita ya Kiislamu kuingia nchini Marekani, imeibua mgogoro na vurugu katika viwanja vya ndege vya nchi hiyo hasa kwa kuwa inawatenganisha watu wa familia moja.
Umasikini ulivyoongezeka nchini Marekani.
Pia limeitaja amri ya Rais Donald Trump dhidi ya uhajiri kuwa ni hatua ya tatu ya kuisambaratisha Marekani na kufafanua kuwa, amri hiyo inayowazuia raia wa mataifa sita ya Kiislamu kuingia nchini Marekani, imeibua mgogoro na vurugu katika viwanja vya ndege vya nchi hiyo hasa kwa kuwa inawatenganisha watu wa familia moja.
Umasikini ulivyoongezeka nchini Marekani.
Likizungumzia udiplomasia wa kigeni wa
Rais Trump, The Guardian limeandika kuwa, kitendo cha rais huyo kufanya
mahusiano na urafiki na viongozi madikteta kama vile Mfalme Salman bin
Abdulaziz Al Saud wa Saudia, ni hatua nyingine inayodhoofisha stratijia
ya Marekani duniani na kwa mujibu wa utafiti mpya wa kituo cha uchunguzi
cha Pew, kati ya nchi 37 kulikofanyika uchunguzi huo, ni asilimia 22 tu
ya watu walionyesha kumuunga mkono Trump katika masuala ya kimataifa.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.