ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, July 20, 2017

BREAKING NEWS: TUNDU LISSU AKAMATWA UWANJA WA NDEGE DAR.

Moja ya Habari zilizotufikia kutoka Dar es Salaam ni kuhusu Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika ‘TLS’ ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria wa CHADEMA, Tundu Lissu kukamatwa na Polisi akiwa Airport Dar es Salaam akielekea Kigali, Rwanda  kwenye kikao cha Halmashauri ya EALS kinachoanza kesho.

Kamanda wa polisi viwanja vya ndege, Martn Ortieno amesema kwamba ni kweli wamemkamata Lissu ambaye pia ni Mwanasheria wa Chadema na kwamba amepelekwa makao makuu ya Polisi.

Hata hivyo, kamanda huyo hakutaja sababu za kukamatwa kwa mwanasheria huyo.

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema,  John Mrema amesema kwamba mwanasheria huyo amekamatwa  jioni hii.

Mrema amesema Lissu amekamatwa na watu waliojitambulisha kwamba ni maofisa wa polisi kutoka Kanda Maalum ya Dar es Salaam.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.