ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, July 12, 2017

BARAZA LA MADIWANI SENGEREMA KUWACHUKULIA HATUA WATUMISHI WAKE.



KUTOKANA NA KUTOKUFIKIA LENGO LA UKUSANYAJI WA MAPATO BALAZA LA MADIWANI HALASHAURI YA WILAYA YA  SENGEREMA LIMEKUSUDIA KUWACHUKULIA HATUA WATUMISHI NA WATAALAMU KATIKA HALMASHAURI HIYO  WAKAOBAINIKA  KUHUSIKA.
Maamuzi hayo yametolewa katika kikao cha tatu cha balaza la madiwani kilichafanyika katika ukumbi wa halmashauri ambapo mh;Evarist  Yanga amesema hatua kali zitachukuliwa kwa watendaji watakao bainika na shutuma hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi mtendaji wa halmashauri  bwana Oscar Kapinga amesema tayari halmashauri imeweka mikakati ya kubaini change cha moto zilizojitokeza kwa kipindi kilichopita na kusababisha kutokuyafikia malengo hayo.
 
Na katika mahojianio maalumu waheshimiwa madiwani mh Robati Madaha ambaye ni diwani  wa kata ya CHIFUNFU na mh Emmanuel Munwanizi wa kata ya Nampulukano wao wamesema kuwa watendaji na wataalamu wa halmashauri hiyo ndio chanzo cha kutokusimamia mapato na kupelekea kutokufikia lengo lililokusudiwa.
Halmashauri ya wilaya ya Sengerema  katika mwaka wa fedha 2016/2017 ilipanga kusanya kiasi sha sh.bilioni mbili na laki sita lakini hadi sasa fedha iliyokwisha kuswanya ni sh.milioni stini na sita,laki mbili therathini na tano na moja 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.