Katibu Mkuu wa ADC, Doyo Hassan amesema kama huo hautakuwa msimamo wa Chadema ,Lissu anapaswa kuomba radhi.
Amesema kauli ya kutaka misaada isitishwe hailengi kuwatakia mema Watanzania.
"Tunadhani matatizo yetu ya ndani ni vema tukapambana nayo kuliko kutangazia ugomvi wako kwa mtu asiyekuhusu.’’
"Kwa kauli hii hizi za Chadema ni wazi wameshindwa mapambano ya ndani na sasa wanafikiria njia nyingine ambazo ni hatari zaidi katika nchi yetu,"amesema Hassan.
Amesema kama Chadema imeshindwa kupambana na CCM na Serikali yake ni wazi wawaeleze wafuasi wao kuliko kutoa matamshi ambayo yanahatarisha ustawi wa taifa letu.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.