Na Abubakari Akida
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano
wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Mwinyi, amesema Serikali itaendelea kutoa
huduma kwa wakimbizi ikishirikiana na mashirika mbalimbali ya ndani na nje ya
nchi, huku akiziomba nchi zenye machafuko kukaa na kutatua changamoto
zinazopelekea watu kukimbia nchi zao.
Akizungumza wakati wa kuadhimisha Siku ya Wakimbizi Duniani,
iliyofanyika katika ukumbi wa Little Theatre jijini Dar es Salaam Balozi Mwinyi
alisema Serikali ya Tanzania imekuwa
ikisaidia masuala ya wakimbizi kutoka awamu ya kwanza ya Muasisi wa Taifa na
Rais wa Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere, ikiwepo kuwapa huduma za afya na elimu
ili waweze kutimiza ndoto zao walizokuwa nazo kabla ya kuzikimbia nchi zao na
kwamba ikiwa leo tunaadhimisha siku ya
wakimbizi duniani lazima wote tudhamirie kumaliza tatizo hili.
“Tuunge nguvu ya pamoja
kuhakikisha tunamaliza migogoro kupitia njia ya mazungumzo ili tuweze kumaliza
tatizo la wakimbizi duniani, na tushirikiane nan chi zinazohifadhi wakimbizi,
mashirika ya kimataifa tukijua jukumu la kutatua changamoto hii ni letu,”
alisema Balozi Mwinyi
Akizungumza kwenye
maadhimisho hayo, Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa (UN) nchini
Tanzania, Alvaro Rodriguez, alisema Umoja wa Mataifa kupitia Shirika la Umoja
wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi
Duniani(UNHCR) limekuja na mkakati maalumu wa kuwahudumia wakimbizi nan chi
zinazohifadhi wakimbizi (CRRF),lengo ikiwa ni kukabiliana na changamoto za kimaendeleo
zinazowakabili wakimbizi katika makambi
mbalimbali.
Naye Mwakilishi wa
UNHCR Tanzania,Chansa Kapaya alisema
shirika lake litaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuhakikisha
wakimbizi wanaendelea kupokea misaada muhimu ya kibinadamu,katika mazingira
ambayo yanawaruhusu kuishi kwa usalama na hadhi.
Tarehe 20 mwezi Juni
dunia inaazimisha Siku ya Wakimbizi Duniani
huku ikikadiriwa kila baada ya sekunde ishirini mtu mmoja hukimbia nchi
yake na kuacha familia, nyumba na mali akikimbia machafuko, migogoro na aina
mbalimbali za uhalifu kwa binadamu na kundi linaloathirika zaidi ni watoto
wadogo wanaokadiriwa kuwa wengi katika idadi ya jumla ya 65.6milioni ya wakimbizi duniani.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.