ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, June 21, 2017

OJADACT YALAANI VIKALI KUFUNGIWA KWA GAZETI LA MAWIO


Mwenyekiti wa OJADACT, akiongea na Waandishi wa Habari juu  ya  msimamo wa chama  kwa  kufungiwa Gazeti la Mawio , leo Jijini Mwanza

Neema Joseph
Mwanza.

 Chama Cha Waandishi wa Habari wa Kupiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uhalifu Tanzania(OJADACT) walaani kufungiwa kwa Gazeti la Mawio.

Akizungumza na waandishi wa habari  leo ofisi za chama  Mwenyekiti  Bw, Edwin Soko amebainisha kuwa, OJADACT wanalaani  kufungiwa kwa  gazeti  la Mawio, kwa kuwa makosa  mawili  yaliyoainishwa  hayana  uzito wa kulifungia Mawio

 kosa la kwanza  Chini ya kifungu cha namba 59 chaa Sheria ya Huduma za Habari 2016,  kwa kuchapisha picha za marais wastaafu na kuwahusisha na kashifa ya rushwa wakati tamko la Rais lilikataza kujadiliwa kwa marais wataafu.

 Kosa la pili Chini ya kifungu cha 38 cha Sheria ya Huduma za Habari 2016, gazeti la Mawio linatuhumiwa kuwa lilichapisha maagizo na maelekezo ya Serikali, lilinukuu kauli yambunge wa Singida Mashariki Chadema Tundu Lissu.

Bwana  Soko, alisema hawajaridhishwa   na sababu zilizotolewa na Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Dr. Harrison Mwakyembe alioutoa Juni 15, 2017 na kulifungia gazeti hilo.

“Hii si mara ya kwanza kwa Gazeti la Mawio kufungiwa, Magazeti mengine yaliyowahi kufungiwa ni, Mwananchi , Mawio, Mwanahalisi na mtanzania kwa kutumia Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976” Alisema Bwana Soko.

Akichambua  makosa  hayo bwana  Soko alisema kuwa,  Kwa mujibu wa kifungu cha 50 (a),(b),(c) ,(d) na (e) na 59 cha Sheria ya Huduma za Habari, mamlaka yenye uwezo wa kufungia Gazeti ni Mahakama na sio Waziri baada ya kumsikiliza mtuhumiwa , hivyo Waziri amekiuka katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, anapaswa afunguliwa kesi ya kukiuka katiba ya  Nchi , pia wakati tamko linatoka gazeti la Mawio lilikuwa limekwisha chapishwa hivyo halikupaswa kuchukuliwa hatua.

Pia  aliongeza kuwa,  Kwa mujibu wa kifungu cha 38 cha Sheria ya Huduma za Habari halina mashiko kwa kuwa, Vyombo vya Habari vina nafasi ya kunukuu mijadala na majadikiano yanayofanyika bungeni na kuyachapisha kwa lengo la kufikisha kinachojadiliwa.

 Huu ni unyimwaji wa Uhuru wa Vyombo vya Habari na haki ya kupata taarifa, kama ilivyoainishwa kwenye ibara ya 18 ya Katiba ya Nchi. Tunawaomba wadau na watanzania wote kuungana na kupinga maamuzi gandamizi dhidi ya vyombo vya habari, Gazeti la Mawio lifungue kesi dhidi ya maamuzi ya Serikali ya kulifungia. , Alisema   Soko

Bwana Soko  ameiomba    Serikali      kufuata sheria za Nchi  ili kuepuka migongano na Wadau wa Habari,  pia iheshimu uhuru wa habari  ni haki ya kikatiba kama ilivyoainishwa kwenye ibara ya 18 ya katiba ya nchi yetu na kama ilivyoainishwa kwenye mikataba ya kikanda, kimataifa,  na kwenye mkataba wa Azimio la Kimataifa la Haki ya binadamu 1948, Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kisiasa na Kiraia (ICCPR), chini ya ibara ya 19, Mkataba wa Aarhus, Azimio la Uhuru wa kujieleza la Afrika 2002 na Azimio la Afrika Juu ya Demokrasia.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.