Taarifa zinasema Ally Yanga alikuwa kwenye msafara wa mbio za Mwenge kabla ya kupata ajali hiyo barabara ya Wiyenzele kuelekea Chipogoro na kufariki hapo hapo. Ally aliyezaliwa mkoani Shinyanga Machi 1, mwaka 1984 katika familia ya watoto sita, kabla ya umauti wake inafahamika alikuwa anaishi Yombo Vituka, Dar es Salaam.
WAKATI HUO HUO:-
Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma Lazaro Mambosasa amethibitisha kifo cha shabiki huyo maarufu wa Yanga, Ally Mohamed aka Ally Yanga kilichotokea leo katika ajali ya gari aina ya Rav4 eneo la Chipogolo wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma.
Ally Yanga ambaye pia ni mkereketwa wa Mwenge wa Uhuru alikutwa na mauti akiwa katika gari la kampun ya Fanikiwa ambalo lilikuwa kwenye promotion na sio kwamba alikuwa kwenye msafara wa Mwenge kama inavyoenezwa.
Lakini tangu baada ya uchaguzi Mkuu Novemba 2015, Ally Yanga ameadimika viwanja vya soka kutokana na kujikita zaidi kwenye shughuli za Chama cha Mapinduzi CCM.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.