Askari wa serikali ya Somalia amehukumiwa
kifo kwa kumuua waziri wa serikali ya Mogadishu baada ya kudhania kuwa
ni mmoja kati ya wanachama wa kundi ya kigaidi la al Shabab.
Afisa
wa jeshi la Somalia, Hassan Ali Noor amesema kuwa, Mahakama ya Kijeshi
ya nchi hiyo imemhukumu kifo askari Ahmed Abdulahi Ahmed kwa kumpiga
risasi na kumuua kimakosa waziri wa serikali.
Abbas
Abdullahi Sheikh Siraji aliyekuwa waziri wa kazi za umma wa serikali ya
Somalia alipigwa risasi akiwa katika gari lake mjini Mogadishu mapema
mwezi Mei.
Siraji
aliyekuwa na umri wa miaka 31 alikulia katika kambi ya wakimbizi wa
Kisomali nchini Kenya na alikuwa waziri mwenye umri mdogo zaidi katika
serikali ya Somalia.
Wapiganaji wa kundi lakigaidi la al Shaba.
Magaidi wa kundi la al Shabab wamekuwa wakishambulia viongozi na
ofisi za serikali ya Somalia na taasisi za kimataifa nchini Somalia na
katika nchi kama Kenya na Uganda.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.