Shirika hilo la kutetea haki za
binadamu limetoa taarifa likitaka kutazamwa upya kwa hukumu ya raia saba
wa nchi hiyo waliohukumiwa kunyongwa. Shirika hilo limetaka kurejeshwa
mafaili ya watuhumiwa hao katika Mahakama Kuu ya nchi hiyo ili ipitie
upya hukumu hiyo.
Sehemu moja ya taarifa ya Shirika la
Msamaha Duniani imebainisha kwamba, kufanyiwa marekebisho sheria
inayozuia kukatiwa rufaa hukumu ya kifo ambayo hivi karibuni
iliidhinshwa na rais Abdul Fatah al-Sisi ni jambo ambalo linaweza
kupelekea kuongezeka hukumu kama hizo na kunyongwa raia wa nchi hiyo.
Mahakama ya Misri
Hayo yanajiri katika hali ambayo, Jumamosi Mahakama moja nchini Misri
iliwahukumu adhabu ya kifo watu 31 kwa tuhuma za kushiriki katika
mauaji ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa zamani wa nchi hiyo.Mahakama ya Misri
Kwa miaka kadhaa sasa Misri imekuwa
ikikabiliwa na machafuko, mauaji, maandamano na mashambulizi katika
pembe mbali mbali za nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika, hasa baada ya
tarehe 3 Julai, 2013 wakati jeshi la nchi hiyo lilipofanya mapinduzi ya
kijeshi yaliyomuondoa madarakani Mohammad Morsi, rais wa kwanza wa Misri
kuchaguliwa kidemokrasia.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.