ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 7, 2017

ZAIDI YA HEKTA KUMI ZA BANGI ZATEKETEZWA NA MKUU WA MKOA WA MZA JOHN MONGELA


NA ZEPHANIA MANDIA WA G.SENGOBLOG,
Mkuu wa mkoa wa Mwz JOHN MONGELA amewapongeza raia wema waliofanikisha kukamatwa na kuteketezwa kwa takriban ekari kumi za bangi ndani ya kipindi kisichozidi mwezi mmoja wialyani Sengerema Mkoani Mwanza.

MONGELA amesema wananchi wamepata hamasa ya kufichua maovu katika jamii kutokana na imani waliyonayo kwa serikali ya awamu ya tano chini ya rais JOHN POMBE MAGUFULI ambayo imekuwa ikifanyia kazi taarifa za siri kutoka kwa raia wema.

Nchi imetangaza vita dhidi ya dawa za kulevya na makamanda wa vita hivyo mkoani mwz wakiongozwa na mkuu wa mkoa huo JOHN MONGELA wamelazimika kutembea zaidi ya kilomita 20 ndani ya msitu wa hifadhi wa Buhindi wilayani Sengerema wakisaka dawa za Kulevya, zikiwa ni siku chache tu tangu kisa kama hicho kugundulika ktk msitu wa Maisome wilayani Sengerema.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwz AHMED MSANGI amesema uchunguzi unaendelea kubaini wamiliki wa mashamba hayo ya bangi.
 
Misitu ya hifadhi imekuwa ikikabiliwa na changamoto kubwa ya uvamizi ambapo watu wamekuwa wakitumia misitu hiyo kama malisho ya mifugo, kuchoma mkaa, kupasua kuni, mbao na mbaya zaidi kilimo cha bangi.










Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.