ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, May 2, 2017

WAWILI WAUWAWA NA FISI SENGEREMA

Mzee anusurika kufa akipambana na fisi aliyevamia zizi la mbuzi Kishapu.

NA ANNASTAZIA MAGINGA, Mwanza

WATU wawili  wa kijiji cha Nyashana Kata ya Kalebezo Wilayani Sengerema wameuwawa  na wengine watano  kujeruhiwa baada ya kuvamiwa  na kushambuliwa na Fisi.



Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza Ahmed Msangi amesema tukio hilo limetokea  May mosi saa 3 asubuhi na kuwataja  Watu hao kuwa ni  Lucia Sinza (65) mkazi  wa Kalebezo na  mtoto mdogo Juma Amos (3) wakati wakiwa shambani alitokea Fisi aliyewavamia na kupelekea kupoteza maisha yao.



Kamanda msangi amesema  kuwa wakati mnyama huyo  akiendelea kumshambulia marehemu Lucia, mtoto wake aitwaye Kefreni  Faida ( umri wake haukufahamia mara moja)ambaye pia alikuwepo shambani hapo  alikwenda kumsaidia mama yake, ndipo Fisi alimuacha mama huyo kisha alimrukia Kefrida na kwamba  kwa bahati mbaya alimng’ata mtoto aliyekuwa  amebebwa mgongoni (Juma Amosi) na kupelekea jeraha kubwa lililosababisha kupoteza maisha.


“ kutokana na  kusikia kelele silizokuwa zikitokea maeneo hayo  Watu na majirani  walifika  eneo la tukio  kwa ajili ya kutoa msaada  lakini pia baadhi yao walijeruhiwa  katika sehemu mbalimbali za miili yao” amesema Msangi



Majeruhi  hao  ni  sostenes kisumu( 25), alijeruhiwa mkono wa kulia na paji la uso,Tekla lunilija  (60), ambaye alijeruhiwa mkono wa kulia, Abeli Wiliam (35), alijeruhiwa mguu wa kushoto pamoja na Musa Nyuma (40), aliyejeruhiwa kisha kutolewa kiganja chote cha mkono wa kulia.



Kamanda Msangi amesema askari walifika eneo la tukio na kushirikiana na wananchi na kisha kufanya msako mkali wa kumtafuta fisi huyo na  hatimaye kufanikiwa kumuuwa na kwamba majeruhi hao wanaendelea na matibabu katika Hospitali ya wilaya ya Sengerema na hali zao zinaendelea vizuri.



Miili ya marehemu tayali imefanyiwa uchunguzi na kukabidhiwa kwa ndugu zao kwaajili ya mazishi na  Kamanda wa Polisi mkoani hapa na Naibu kamishina wa Polisi Ahmed Msangi ametoa pole kwa ndugu jamaa na marafiki waliopatwa na msiba huo, huku akiwaomba wananchi kuwa makini pindi wanapokuwa katika maeneo ya mashambani dhidi ya wanyama wanaoweza kuhatarisha maisha yao.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.