ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 18, 2017

TANZANIA MACHO YAO YOTE LEO YAELEKEZWA GABON.

GABON:- Timu ya soka ya vijana ya Taifa leo Alhamisi inatarajiwa kukata kiu ya Watanzania kwenye mchezo wake wa pili katika mashindano ya Afrika.

Mchezo wa kwanza, Serengeti Boys iliishangaza Mali baada ya kutoka suluhu ya 0-0.

Timu hiyo mpaka sasa imefikisha pointi moja na matokeo mazuri ya leo inaweza kuifanya kusogea hadi nafasi ya kwanza kwenye kundi B.
Picha kwa hisani ya Wapenda soka.

Macho na masikio ya Watanzania yataelekezwa kwenye runinga zao, huku wakiiombea dua ili iweze kushinda ili kusonga mbele katika mashindano hayo yanayoendelea nchini Gabon.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.