Mazishi ya aliyekuwa mwenyekiti wa uwt wilaya ya Sengerema
ambae pia ni diwani mstaafu viti maalumu kwa tiketi ya CCM yamefanyika JANA
katilka kijiji cha Nyabutanga katika Halmashauri ya Buchosa .
Akizungumzia wasifu wa marehemu Stefania Shindika katibu wa CCM mkoa wa Mwanza mwl Raymond
Steven Mwangwala amesema kuwa chama kimempoteza mtu muhimu kwakuwa alikuwa mstari
wa mbele kuwaunganisha wanawake katika wilaya ya Sengerema
BOFYA PLAY KUSIKILIZA.
Kwa upande wake m/kiti UWT mkoa wa Mwanza bi ELEN MAKUNGU
amesema kuwa marehemu Stefania Shindika alikuwa chachu ya maendeleo kwa
wanawake wa mkoa wa Mwanza.
Marehemu Stefania
Shindika alizaliwa mwaka 10/10/1958 katika kijiji cha Kimuli wilaya ya
Karagwe mkoani Kagera, na amewahi kufanaya kazi katika CHAMA CHA USHIRIKA WA WAKULIMA (NYANZA)
, mwaka 1975 alijiunga na chama cha Tanu na kasha kuhamia CCM mwaka 1977 ,mwaka
2005 marehemu Stefania alichaguliwa kuwa diwani viti maalumu kata ya nyakalilo
mwaka 2012 alichaguliwa kuwa m/kiti UWT wilaya ya Sengerema.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.