Kwa akali watu wawili wameuawa na wengine
watatu wamejeruhiwa katika mripuko wa bomu la kuendeshwa kutokea mbali
katika viunga vya mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
Hayo yameelezwa na tovuti ya
habari ya Garowe na kuongeza kuwa, basi la abiria jana Jumapili
lilikanyaga bomu hilo lililokuwa limetengwa barabarani katika eneo
la Garasbaley, yapata kilomita 9 magharibi mwa Mogadishu na kusababisha
maafa hayo.
Mashuhuda wa mripuko huo wamesema
kwamba, hujuma hiyo ilikuwa imelenga msafara wa magari ya jeshi ambao
ulikuwa unapita katika eneo hilo. Habari zaidi zinasema kuwa,
waliojeruhiwa katika shambulizi hilo akiwemo mwanamke mmoja wanatibiwa
katika hospitali moja mjini Mogadishu.
Hadi tunaenda mitamboni, hakuna kundi
lololote lililokuwa limekiri kuhusika na hujuma hiyo ya bomu, ingawaje
kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab ni maarufu kwa kufanya
mashambulizi ya aina hii.
Magaidi wa al-Shabaab wamekuwa wakifanya
mashambulizi dhidi ya misafara ya magari jeshi na Kikosi cha Kusimamia
Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM inayotumia barabara kuu
ya Mogadishu kuelekea katika wilaya ya Afgoye na maeneo mengine ya nchi.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.