ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 6, 2017

TANZANIA YANG'ARA VIWANGO VYA FIFA, YAPANDA NAFASI 22 JUU.

TANZANIA imepanda Kwa nafasi 22 kwenye viwango vya FIFA duniani kutoka nafasi ya 157 kwa mwezi wa pili na sasa imeshika namba135. Hii inatokana na Stars kufanya vizuri kwenye mechi mbili za kirafiki dhidi ya Botswana waliyoshida kwa magoli 2-0 na Burundi iliyoshinda kwa magoli 2-1.

Pia Brazil imeipiku Argentina kwenye nafasi ya kwanza kwa mwezi wa tatu Argentina ilikuwa nafasi ya kwanza kwa mwezi wa pili huku Brazil wakiwa nafasi ya pili. Haya ndio mataifa kumi yanayoongoza kwenye viwango vya soka Duniani 1. Brazil 2. Argentina 3. Germany 4. Chile 5. Colombia 6. Ufaransa 7. Ubeligiji 8. Ureno 9. Uswisi na 10. Hispania.

Mataifa 10 yanayongoza Afrika, kwenye mabano ni nafasi zao za viwango vya ubora duniani.

1. Misri (19) 2. Senegal (30) 3.C ameroon (33) 4. Burkinafaso (35) 5. Nigeria (40) 6. DR Congo (41) 7. Tunisia (42) 8. Ghana (45) 9. Ivory Coast (48) 10. Morocco (53)

Kwa Afrika Mashariki Uganda inaendelea kuongoza ikiwa nafasi 72 ikiwa imepanda nafasi 3 kutoka 75 ya mwezi wa Pili, Kenya nafasi 78 nayo ikiwa imepanda Kwa nafasi 10 kutoka 88 ya Mwezi uliopita wakati Rwanda yenyewe inakamata nafasi ya 117 ikiwa imeshuka kwa nafasi 17 kutoka nafasi ya 100 ya mwezi uliopita na Burundi ambao ilifungwa na Tanzania ipo katika nafasi ya 141 nayo ikiwa imeporomoka kwa nafasi 3 kutoka nafasi ya 138 ya mwezi wa pili.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.