ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, April 24, 2017

MTATIIRO AJA NA YAKE KATIKA SAKATA LA CUF NA TIMBWILI LAO LENYE NYINGI SINTOFAHAMU.

Kutoka kwenye ukurasa wa Facebook wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Muda wa CUF bwana Julius Mtatiro

"Mwanasheria Mkuu wa chama chetu, Wakili Msomi HASHIM MZIRAY yuko katika kituo cha Polisi Magomeni ambako amemsindikiza Mwenyekiti wetu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Juma Mkumbi.

Mhe. Juma Mkumbi ndiye aliyevamiwa na Mungiki wa Lipumba, akiwa anaongoza Mkutano na vyombo vya habari pale Vina Hotel. Polisi walipofika wakamshauri arejee nyumbani akapumzike (ana diabetes) kisha wakamshauri akaripoti kituoni jana kwa ajili ya ku LODGE malalamiko yake rasmi ili yaunganishwe na malalamiko ya waandishi wa habari na viongozi waandamizi waliovamiwa juzi.

Jana mhe. Mkumbi alishindwa kwenda kufungua kesi kwani hali yake ya afya haikuwa nzuri na leo ndipo alipanga kwenda. Ikumbukwe pia simu za jana za OCD na OCCID za kutaka kuwapatanisha na wale wavamizi.

MAAJABU YA DUNIA...
Leo amekwenda Magomeni Polisi ili kuripoti tukio zima lilivyokuwa (kwani Juzi Polisi walichukua maelezo ya wanahabari na viongozi waandamizi tu wale waliokuwa wamepigwa, kuumizwa au kujeruhiwa).

Mkumbi amefika Magomeni Polisi ili kufungua mashtaka yake kama muathiriwa lakini OCD na OCCID wa Magomeni wameelekeza ahojiwe kama Mtuhumiwa. Hivi tuzungumzavyo Juma Mkumbi ndiye anahojiwa kwa tuhuma za kumjeruhi yule MUNGIKI aliyekatwa mguuni na Wananchi (Mlinzi wa Lipumba).

MAELEKEZO WALIYOPEWA POLISI..
Niliwaeleza hapa, kwamba Polisi wameelekezwa wahakikishe aidha upande ULIOVAMIWA (Chama) unakubali kukaa meza moja na wale WALIOVAMIA (Lipumba na Mungiki) AU Upande wa chama ndiyo unapewa kesi ya kujeruhi lile jambazi lililojeruhiwa na wananchi.

HURUMA INAPONZA
Wananchi wenye hasira walipokuwa wanaliadhibu "ZOMBI" lile, liliokolewa na viongozi wale wale walioshuka haraka chini na kuomba waitwe polisi. Yaani, kama si juhudi za kina Juma Mkumbi na wenzao, zombi la Lipumba lingeliuawa. Huruma yao kuingilia kati na kulikokoa na wakaita polisi likakamatwa, ndiko kumewaponza. Polisi wanatufundisha kuwa the next person wa Lipumba ambaye atatuvamia basi viobgozi waache auawe maana wakimsaidia wao wanageuziwa kibao. Sawa tumeelewa somo!

BASTOLA
Hadi sasa, polisi hawaelezi lile ZOMBI lililokuwa na Bastola liko wapi na hawasemi ile bastola iko wapi pia. Kwa kifupi Polisi hawataki kuzungumzia masuala ya Bastola ile. Badala ya kushughulikia mambo makubwa, sasa wana-deal na upande wetu.

WITO
Natoa wito kwa wanachama wa CUF kukaa STANDBY, tunataka kuona Zombi/Mungiki lililokamatwa na wananchi linafikishwa mahakamani.

Tunataka kuona wale wote waliokuwa na Zombi hilo wanakamatwa pia na kufikishwa mahakamani. Wanafahamika kwa majina, kwa sura na kwa makazi.

Tunataka kuona ile BASTOLA inasakwa na aliyekuwa nayo anapatikana. Uzuri aliyekuwa na bastola alipanda kwenye yale magari mawili yaliyotumika kwenye uvamizi.

Tunataka kuona magari yaliyotumika kwenye uvamizi ule yakikamatwa NA madereva wa magari yale (wanafahamika) wanakamatwa haraka.

Tunataka kuona mkuu wa wavamizi wale anakamatwa haraka na jana alionekana AZAM TV akitamba kuwa mazombi yake yataendelea na oparesheni ya kuvamia na kupiga watu, (na polisi wana clips zote).

Kwa sababu leo tumekutana na Kamishna Sirro tunajipa muda kuona hatua zipi zitachukuliwa. Kama hatua hazichukuliwi na Polisi, basi, sisi tutawaambia wanachama wetu WASIFE KIKONDOO huko mitaani, tutawaomba wajilinde kwa nguvu zote kwani hiyo ni haki yao ya kikatiba. Kile kijikundi cha MUNGIKI na LIPUMBA kina watu wachache sana, lakini UJINGA wetu ni kuendelea kuheshimu sheria za nchi.

Mtatiro J,
24 April 2017."

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.