ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 14, 2017

KENYA YATAHADHARISHA JUU YA UWEZEKANO WA KUFANYIKAMASHAMBULIZI YA KIGAIDI.


Vyombo vya usalama vya Kenya vimetahadharisha juu ya uwezekano wa kufanyika mashambulizi ya kigaidi nchini humo. 
George Kinoti Msemaji wa Polisi ya Kenya alisema jana usiku kuwa tayari kumesambazwa taarifa kwamba magaidi tisa wanafanya kila linalowezekana kutekeleza mashambulizi ya kigaidi nchini humo.

Magaidi wamekuwa wakifanya mashambulizi katika maeneo mbalimbali ya serikali huko Kenya baada ya kupata pigo mbele wanajeshi wa Kenya. Kundi la kigaidi la al Shabab lenye makao yake Somalia limekuwa likifanya mashambulizi na hujuma mbalimbali katika ardhi ya Kenya; jambo linalowatia wasiwasi viongozi wa serikali ya Kenya.

Shambulio dhidi ya basi la abiria lililofanywa na al Shabab huko Kenya mwaka jana
Aidha wiki iliyopita wanamgambo 15 wa kundi la kigaidi la al Shabab waliuawa katika mapigano na wanajeshi wa Kenya katika eneo la Gedo kusini mwa Somalia. eneo hilo ni eneo la mpaka wa pamoja kati ya nchi mbili hizo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.