ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 7, 2017

Burundi: WAPIGANAJI WA KAGAME NDIYO WALIOTUNGUA NDEGE ALIYOKUWA AMEPANDA CYPRIEN NTARYAMIRA, RAIS WA ZAMANI WA BURUNDI.

Mabaki ya ndege aliyokuwa ameipanda rais huyo wa zamani wa Burundi aliyeongoza kwa miezi miwili pekee.
Serikali ya Burundi imeadhimisha hapo jana mwaka wa 23 tangu kuuawa kwa Cyprien Ntaryamira, rais wa zamani wa nchi hiyo. 

Ntaryamira alipoteza maisha katika ajali ya ndege kwenye anga ya mji wa Kigali, Rwanda ambayo hata hivyo serikali ya Bujumbura imeitaja kuwa ilifanywa na wapiganaji wa Rais Poul Kagame wa Rwanda.
  
Hii ni mara ya kwanza kwa serikali ya Bujumbura kuituhumu moja kwa moja serikali ya Kigali kuhusika katika tukio hilo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.