Viongozi wa wa Ligi ya Premier
Chelsea walipiga hatua kubwa kuelekea kushinda ligi baada ya kuwanyuka
Everton mabao matatu kwa nunge.
Mabao yote ya Chelsea yalifungwa katika kipindi cha pili.Ina maana kuwa hata kama Chelsea itashuka kwa pointi tatu kwenye mechi nne zilozosalia bado itachukua nafasi ya pili kwa miaka mitatu mfululizia hata kama Tottenham watashinda mechi zote zilizosalia.
Iliwalazimu Chelsea kusubiri kabla ya kombora ya Petro lililotumbukia wavuni mnamo dakika ya 66.
Everton walikuwa wameanza kwa kasi kwa mwendo wa kazi ambapo Dominic Lewin nusura afunge.
Sare ya Manchester City na Middlesbrough ina maana kuwaa klabu yake Ronald Koeman iko nyuma kwa pointi nane kutoka kwa klabu nne za kwanza huku ikibaki na mechi tatu tu.
Mshambuliaji wa Manchester United, Marcus Rashford akienda chini baada
ya kuangushwa na kipa wa Swansea City, Lukasz Fabianski na refa Neil
Swarbrick kuamuru penalti ambayo ilifungwa na Wayne Rooney kuipatia timu
yake bao la kuongoza dakika ya 45 na ushei katika mchezo wa Ligi Kuu ya
England Uwanja wa Old Trafford, kabla ya wageni kusawazisha kupitia kwa
Gylfi Sigurdsson dakika ya 79.
VIDEO
VIDEO
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.