ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, March 8, 2017

VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI YA ENGLAND BAADA YA ARSENAL KUCHEZEA 10


Arsenal walibomolewa na Bayern Munich kwa mara nyingine tena na kujikuta wakitolewa katika michuano ya Klabu Bingwa Ulaya katika ngazi ya timu 16 kwa kuzabwa jumla ya magoli 10-2.
Arsene Wenger, ambaye atakuwa chini ya shinikizo kali kufuatia kichapo hiki, alishuhudia timu yake ikifungwa magoli 5-1, baada ya kuongoza kwa kupitia bao lililofungwa na Theo Walcott katika kipindi cha kwanza.

Kichapo cha magoli 5-1 kwenye uwanja wa Emirates walichotoa Bayern Munich kwa Arsenal ndio habari ya ‘mujini’ kwenye kurasa za habari za michezo za magazeti mengi ya England.
Kila gazeti limeipa uzito habari hiyo ambayo imeitikisa dunia hasa matokeo ya jumla (aggregate) kuwa Bayern Munich 10-2 Arsenal.

Arsenal imeweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza England kuondoshwa kwenye michuano ya UEFA Champions League kwa kichapo kikubwa zaidi.



Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.