ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, March 8, 2017

UWANJA WA NDEGE WA ABUJA, NIGERIA KUFUNGWA KWA WIKI SITA; KADUNA KUTUMIKA KAMA MBADALA.


SERIKALI ya Nigeria imetangaza kuwa, uwanja wa ndege wa mji mkuu Abuja utafungwa kuanza leo Jumatano kwa muda wa siku sita ili kupisha ukaratabati wa barabara za kukimbilia ndege. 
Msemaji wa Wizara ya Anga ya Nigeria amesema kuwa, hatua hiyo imechukuliwa baada ya mashirika kadhaa ya ndege kusitisha kutua ndege zao katika uwanja huo.
Taarifa ya Wizara ya Anga ya Nigeria imesema kuwa, sasa wasafiri wanaotumia uwanja huo watahamishiwa katika uwanja wa ndege wa Kaduna uliopo yapata kilomita 160 kaskazini mwa mji mkuu Abuja.
Wasafiri hao watasafirishwa kwa mabasi na misafara yao kusindikizwa na askari wa kikosi cha ulinzi kutokana na miaka ya hivi karibuni kushuhudiwa vitendo vya utekaji nyara katika njia ya kuelekea Kaduna.
Barabara ya kukimbilia ndege katika Uwanja wa Ndege wa Abuja.
Serikali ya Nigeria imesema kuwa, inatumai mashirika ya ndege ya kimataifa yatakubali kuutumia uwanja wa ndege wa Kaduna kama mbadala hadi ukarabati wa uwanja wa Abuja utakapokamilika. Hata hivyo mashirika kadhaa ya ndege ya kimataifa yakiwemo ya British Airways, Lufthansa na la Afrika Kusini yametangaza kuwa hayatatumia uwanja wa ndege wa Kaduna.
 
Hadi sasa ni Shirika la Ndege la Ethiopia tu la Ethiopian Airlines ndilo lililotangaza kuwa, liko tayari kuutumia uwanja wa ndege wa Kaduna.
Baada ya kuweko habari za kugongana kuhusiana na siku hasa ya kufungwa uwanja wa ndege wa Abuja, James Odaudu msemaji wa Wizara ya Anga ya Nigeria amethibitisha kuwa, uwanja huo utafungwa kuanzia leo Jumatano.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.