ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, March 27, 2017

MAZUNGUMZO YA KUPIGA MARUFUKU SILAHA ZA NYUKLIA YAANZA NEW YORK, MAREKANI.


Mazungumzo ya kupiga marufuku silaha za nyuklia yameanza mjini New York Marekani bila ya kuwashirikisha wajumbe kutoka Russia, Marekani, Ufaransa na Uingereza. 
Shirika la habari la IRNA limeripoti  kuwa makao makuu ya Umoja wa Mataifa huko New York kuanzia leo Jumatatu hadi tarehe 31 mwezi huu yatakuwa mwenyeji wa mazungumzo yanayohusu uandaaji wa mkataba unaopiga marufuku na kutaka kuangamziwa kikamilifu silaha za nyuklia, mazungumzo ambayo yanafanyika bila ya kushiriki wajumbe kutoka Russia, Marekani, Uingereza na Ufaransa ambazo ni kati ya madola yanayomiliki nguvu za nyuklia duniani.
Kombora la nyuklia la Marekani.

Uamuzi huo wa kuandaa rasimu ya mkataba huo ulichukuliwa mwezi Disemba mwaka jana na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Nchi zaidi ya 100 zimeunga mkono azimio linalounga mkono kuandaliwa rasimu ya mkataba wa kupiga marufuku silaha za nyuklia, hata hivyo Russia na nchi nyingine 35 wanachama wa Umoja wa Mataifa zimepinga azimio hilo.
Madola yanayomiliki silaha za nyuklia duniani zikiwemo Russia na Marekakani zimepinga wazo hilo la kupasisha mkataba unaozuia uundaji silaha za nyuklia.
   Hii ni katika hali ambayo, madola makubwa duniani yaani nchi tano wanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa zingali zimeazimia kumiliki maghala yao ya silaha za nyuklia, licha ya kuwepo jitihada za kimataifa za kupunguza maghala ya silaha za nyuklia khususan kuwepo mkataba unaopiga marufuku uenezaji na usambazaji wa silaha hatari za nyuklia (NPT).

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.