ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 4, 2017

IGP MANGU AKEMEA DAWA ZA KULEVYA.

Mgeni rasmi Afande IGP Ernest Mangu akikagua vikosi mbalimbali vya jeshi la polisi mkoa wa Mwanza katika sherehe ya kukabidhi vyeti vya heshima kwa baadhi ya askari waliofanya vyema kipindi cha mwaka 2016-2017. Shughuli ikifanyika katika viwanja vya polisi mabatini.
Akizungumza na askari polisi jijini Mwanza wakati akiwatunuku askari 30 waliofanya vizuri kutoka katika wilaya 7 mkoani hapa Mkuu huyo wa jeshi hilo amesema hatua kali zitachukuliwa dhidi ya mtu yeyote atakayejihusisha na vitendo hivyo bila kujali cheo chake.

“Mapambano ya dawa za kulevya si nguvu za soda ni mapambano endelevu tumetamka ,kwahiyo tu watupe ushirikiano na wale wanaobeza pengine ndiyo watumiaji wenyewewa dawa za kulevya au wanufaikaji, kwahiyo tunaomba waache hiyo biashara haramu,” alisema IGP Mangu.
 

VIDEO YA TUKIO.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.