SHIRIKA la Msalaba Mwekundu limesema Kenya
inahitajia msaada wa dharura wa chakula ili kunusuru maisha ya watu
milioni 3 wanaokabiliwa na hatari ya kufa njaa kutokana na kushtadi
ukame nchini humo.
Dakta Abbas Gullet, Katibu Mkuu wa shirika hilo amesema kuwa,
hali ya kibinadamu katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki inazidi kuwa
mbaya kutokana na kutonyesha mvua za kutosha, huku watoto wakiwa wahanga
wakuu wa janga hilo.Amesema kuwa, watoto zaidi ya laki 3 na 40 elfu walio chini ya umri wa miaka mitano wanakabiliwa na utapiamlo wa kiwango cha juu na kusisitiza kuwa, iwapo hatua za dharura hazitachukuliwa, yumkini watapoteza maisha karibuni hivi.
Athari hasi za ukame. Watoto wanakabiliwa na utapiamlo wa kiwango cha juu. |
Sambamba na tangazo hilo lililotolewa na Ofisi ya Rais Uhuru Kenyatta, Kenya ilizitaka taasisi za ndani na za kimataifa kuisaidia serikali ya Nairobi katika juhudi zake za kukabiliana na athari mbaya zilizosababishwa na ukame.
Hivi karibuni Shirika la Msalaba Mwekundu lilitahadharisha kwamba, watu zaidi ya milioni 11 katika nchi za Kenya, Ethiopia, Somalia na Sudan Kusini wamo katika hatari ya kufa njaa na wanahitaji kwa haraka msaada wa kibinadamu, kutokana na kukithiri kwa ukame.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.