ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 17, 2017

WAZEE HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA WAKUMBUKWA

Halmashauri ya wilaya ya Sengererma imezindua vitambulisho kwa wazee ili kupata matibabu bure

Akizungumza na wazee hao  katika kata ya IGALULA wilayani humo  mkuu wa wilaya ya Sengerema mh Emanuel Kipole amewataka wananchi kufanya kazi ilikuleta maeendeleo ya taifa kwa kuwa serikali ya awamu ya tano inawataka watu wafanye kazi.

cue in MH KIPOLE 01 KAZI

Mh kipole amewapongeza wazee hao  na  kusema kuwa serikali inatambua mchango wa wazee na busara pia katika kulitumikia taifa na hata kupigania uhuru hivyo itaendelea kuwaenzi wazee  hasa upande wa afya kwakuwa mtaji mkubwa wa maisha ya mwanadamu ni afya.e
  
Akizungumzia mpango wa serikali kwa wazee  mh.Kipole amsema kuwa wazee wote kuanzia umri wa miaka 60 serikali itahakikisha wanapata huduma za afya bure bila malipo ,na zoezi hili la vitambulisho  limeanza mwaka jana na tayari wazee 2001 wamekisha kupatiwa  vitambulisho na bado linandelea.

Akimkaribisha mgeni rasmi Mkurugenzi wa wilaya ya Sengerema  Magesa Mafuru  Bonifasi amesemakuwa zoezi hili nimefanyika kwa ufanisi, na kufanikiwa kuwahamasisha  wazee 651 na wazee 51 watakabidhiwa vitamburisho kwa kuwawakilisha wazee wengine katika kata nyingine na kuongeza kuwa katika zoezi hili mabalaza mbali mbali yameundwa kuanzia kijiji ,kata na mbalaza la wazee la wilaya.

Naye mganga mkuu  wilaya Sengerema Dr .Petel Mangu amesema kuwa kazi hii ni kutekeleza maelekezo ya serikali kwa kuanzisha baraza na kutengeneza kumbukumbu za wazee katika wilaya na kuwapatia vitamburisho kwa huduma za matibabu na tayari wamefanikiwa kuunda baraza la wazee kwa ngazi ya  kijiji na kata wakichuchumilia ngazi ya wilaya. 

Idara ya afya Halmashauri ya Sengerema imepanga kutengeneza vitamburisho 651 kwa miezi 6, na kwamiezi zita ijayo vitatengenezwa vitamburisho 651 na vitamburisho vilivyotengenewa ni kwa kata 13 kati ya kata 26.

Nao wazee wametoa maoni yao kwa kuipongeza serikali kwa kuwaajali wazee changamoto ni upatikanji wa dawa katika hospitali 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.