ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, February 7, 2017

WANAWAKE WAWILI WAKAMATWA NA BHANGI KILO 110

NA ANNASTAZIA MAGINGA, Mwanza
WANAWAKE wawili wanashikiliwa na Jeshi la polisi Mkoani hapa baada ya kukutwa  wanasafirisha  bhangi kilo 110 kwa ajili ya kuuza kinyume na Sheria.


Tukio hilo limetokea juzi February 5 mwaka huu saa  8 mchana kwenye kizuizi cha mamlaka ya mapato (TRA)Wilayani Magu ambapo Jeshi la lilitiliashaka gari namba T349 DBA aina Tata mali ya Msolasa lilokuwa likitokea Sirari kwenda Mwanza na kulisimamisha kisha kulifanyia upekuzi  na kumkamata Angelina Patrick (50) Mkazi wa Sirari akiwa na bhangi kilo 40 zilizokuwa zimefungwa kwenye marobota manne.


Akizungumza na waandishi wa habari jana Naibu Kamishina wa polisi Ahmed Msangi Mtuhumiwa mwingine ni Frola Lucas (65) Mkazi wa Sirari alikamatwa kwenye gari T.834 CZH aina ya Yutong mali ya kampuni ya Africa Raha lilokuwa likitokea  na kukamata kilo 70 zikiwa zimefungwa kwenye marobota manne ndani ya masunduku matatu.

Aidha watuhumiwa wapo katika mahojiano na Jeshi la polisi na kwamba uchunguzi utakapokamilika watafikishwa mahakamani huku askari wakiendelea na ukamataji wa magari wanayoyatilia shaka  katika maeneo hayo.


Hata hivyo Kamanda Msangi  amewataka  wamiliki wa vyombo vya Moto kuacha tabia ya kujihusisha na usafirishaji  Bhangi kwani ni kosa na endapo ikibainika hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa dhidi yao huku akiwataka wananchi wa Mkoa wa Mwanza kutoa ushirikiano ili kutokomeza biashara yao.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.