ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 10, 2017

TADB YAANZA KUTEKELEZA MKATABA WA USHIRIKIANO KATI YA TANZANIA NA MOROCCO


 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TAD, Bw. Francis Assenga (Katikati) akiwa na Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha, Bw. Albert Ngusaru (Watatu kushoto) wakiwa na wenyeji wao Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Morocco (GCAM).
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) Bw. Francis Assenga (wa pili toka kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na mwenyeji wake Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kilimo ya Morocco (Credit Agricole) Bw. Jamal Eddine Wl Jamali (Katikati). Wengine ni Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha wa TADB  Bw. Albert Ngusaru na Wakurugenzi wawili wa Benki ya Credit Agricole Bi. Dkhil Mariem (Kushoto) na Bi Leila Akhmisse (Kulia).

 Ujumbe wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ukipatiwa maelezo juu ya miradi ya kilimo inavyoendeshwa nchini Morocco wakati Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB Bw. Francis Assenga (Mwenye Kaunda Suti) na Bw. Albert Ngusaru Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha (Mwanye Daftari) walipotembelea Morocco wiki hii kuanza utekelezaji wa Mkataba wa Ushirikiano kati ya TADB na GCAM.
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania Bw. Francis Assenga (Katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Credit Agricole na Tamwil El Fellah wakati walipokagua miradi mbalimbali ya kilimo na ufugaji katika vijiji vya mji wa Khemisset nchini Morocco jana. Kulia kabisa ni Bw. Albert Ngusaru ambaye ni Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha wa TADB.

 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) Bw. Francis Assenga (kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na mwenyeji wake Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kilimo ya Morocco (Credit Agricole) Bw. Jamal Eddine W. Jamali (Katikati). Kulia ni Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha wa TADB  Bw. Albert Ngusaru.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Bw. Francis Assenga (Kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha wa TADB  Bw. Albert Ngusaru (Kulia) walipotembelea Benki ya Kilimo ya Morocco (Credit Agricole).



Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imeanza kutekeleza kwa vitendo Mkataba wa Ushirikiano uliosainiwa kati ya Serikali ya Tanzania na Morocco wakati wa Ziara ya Mfalme wa Morocco Mtukufu Mohammed VI alipotembelea Tanzania kwa mwaliko wa Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli mnamo mwezi Oktoba 2016.

Katika kutekeleza makubaliano hayo, ujumbe wa TADB ukiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Bw. Francis Assenga na Mkurugenzi wa Hazina na Utafutaji Fedha, Bw. Albert Ngusaru upo nchini Morocco, pamoja na mambo mengine kuainisha maeneo ambayo Benki hiyo itashirikiana na Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Morocco (GCAM) na kuwekeana mikakati ya utekelezaji.

Kwa mujibu wa Bw. Assenga, pamoja na kupanga mikakati hiyo, ujumbe huo ulipata fursa ya kukagua miradi kadhaa ya kilimo na ufugaji ambayo Tanzania inaweza kuianzisha kwa mafanikio.

TADB imeanzishwa kwa malengo makuu ya Kusaidia upatikanaji wa utoshelezi na usalama wa chakula ambao ni endelevu nchini Tanzania; na Kuchagiza na kusaidia Mapinduzi ya Kilimo kutoka   kilimo cha kujikimu kwenda cha kibiashara ili kuchangia kwenye ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.