ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 10, 2017

KITUO CHA RADIO SENGEREMA CHAKABIDHIWA KWA HALMASHAURI YA WILAYA YA SENGEREMA

NA OSCAR
JEMBE FM
SENGEREMA
Mkuu wa wilaya ya sengerema mh Emanueli Kipole jana amekabidhi kituo cha radio Sengererma kwa almashauri ya wilaya ya Sengerema kuratibu kituo hicho ambacho ni mali ya serikali kupitia wananchi wa wilaya hiyo.
.
Tendo hilo limefanyika katika ukumbi wa almashauri ya wilaya ya sengerema  katika kikao cha madiwani wa almashauri hiyo  kilichokaa ili kupanga bajeti ya almashauri hiyo.


Mh Kipole amesema kuwa kituo hicho ni mali ya wananchi na kutokana na michango iliyotolewa na almashauri na pia kutika wahisani mbalimbali wakati wa kuanzishwa kituo hicho na serikali haijawahi kukabidhi kituo hicho isipokuwa kuna watu wachache wamejimilikisha kituo hicho.

Inatajwa kuwa umiliki wa kituo hicho tangu mwaka 2005 ulikuwa chini ya kamati ya watu 20 ambao walikuwa wakitumia jina la Halmashauri kuomba misaada toka kwa wahisani na wafadhili mbalimbali wakitengenezamiradi na kujinufaisha ikiwa ni pamoja na kugawana faida wakati Halmashauri haiingizi chochote.

Mhe. Kipole ameunda kamati mpya ya kuiendesha redio hiyo ambapo sasa ofisi zake zinalindwa na jeshi la polisi.

Hata hivyo kikao hicho kimeshindwa kupitisha bajeti hiyo iliyopendekezwa sh 55,466,009,060/= kutokana na kuwa chini ya kiwango cha makusanyo kulingana na vyanzo vya mapato katika almashauri hiyo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.