ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, February 19, 2017

KAMPUNI YA BIMA YA UAP TAWI LA MWANZA YAOSHA MAGARI YA WATEJA WAO BURE ZOEZI KUMALIZIKA LEO.

Mkuu wa Masoko wa Kampuni ya BIMA ya UAP Raymond Komanga.
KAMPUNI ya Bima ya UAP tawi la Mwanza imeamua kuchukuwa jukumu la kuosha magari ya wateja wao wote wa Mwanza bure.

Zoezi hilo limeanza jana Jumamosi tarehe 18 na litadumu kwa muda wa siku mbili hadi leo Jumapili tarehe 19 February saa kumi na mbili jioni.

TMS Car Wash au kwa Makaptura ndo eneo ambalo limepewa dhamana ya kuosha magari ya wateja walio mkoani Mwanza, hawa jamaa wakipatikana ndani ya eneo la uwekezaji la Rock City Mall Kirumba.

Raymond Komanga ambaye ni Mkuu wa Masoko wa Kampuni ya BIMA ya UAP anasema kuwa lengo la kufanya zoezi hili ni kuwashukuru wateja wao wa Mwanza kwa ushirikiano wao kibiashara kwa takribani miaka mitatu tangu tawi lilipofunguliwa.
BOFYA PLAY KUMSIKILIZA

Usafi Zaidi kwa mchuma wako mpaka ung'are kwa hisani ya Kampuni ya BIMA ya UAP.

Wadau wa Kampuni ya BIMA ya UAP pamoja na wadau wa kituo cha uoshaji magari cha TMS kikazi Zaidi.

Mkuu wa Masoko wa Kampuni ya BIMA ya UAP Raymond Komanga akizungumza nasi.
"UAP ambayo ni kampuni yenye mtaji kubwa kuliko zote za Bima Tanzania in
wahakikishia watanzania kuwa wana uwezo wa kulipa madai ya wateja kwa haraka Zaidi" Alisema Komanga.

 "Tangu kuingia sokoni miaka mitatu na nusu iliyopita tumeweza kupanda hadi nafasi ya nne kati ya makampuni ya bima 31 yaliyoko Tanzania"

Pia tumefungua matawi saba nje ya Dar es salaam na Mwanza ikiwa na tawi mojawapo katika barabaraya Pamba.


TMS Car Wash au kwa Makaptura ndo eneo ambalo limepewa dhamana ya kuosha magari ya wateja walio mkoani Mwanza, hawa jamaa wakipatikana ndani ya eneo la uwekezaji la Rock City Mall Kirumba. BOFYA PLAY KUMSIKILIZA
Mmoja wa mabalozi wa Masoko wa Kampuni ya BIMA ya UAP akitoa darasa kwa wamiliki wa magari waliofika mahala hapa kwaajili ya kuoshewa magari yao.
Ze Muonekano na selfie.
Eneo la huduma.
UAP na wewe.
TMS Car Wash Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.