ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, January 31, 2017

BOMBARDIER YASHINDWA KURUKA MARA MBILI JIONI HII KUTOKA AIRPORT MWANZA.

ABIRIA waliokuwa wakisafiri kwa ndege aina ya Bomberdier TC 103 ya Shirika la ndege la Tanzania ATC kutoka Mwanza kwenda jijini Dar es salaam wameshindwa kuruka mara mbili na kulazimika kubaki mjini hapa.

Katika uwanja wa ndege wa Mwanza kuna malumbando baina ya wadau wafanyakazi wa ndege hiyo sanjari na abiria ambao wanataka majibu ya haraka kujua hatma ya safari yao.

Ndege hiyo iliruka kwa takribani dakika 20 na kisha kulazimika kutua kwa dharura hali iliyozua taharuki kwa abiria waliokuwa ndani ya ndege hiyo.

Tayari Ofisa Habari wa ATCL Lily Fungamtama amekiri kutokea kwa tatizo hilo na kusema kuwa  ndege hiyo iliruka lakini ililazimika kutua kutokana na tatizo la kiufundi.

"Baada ya Rubani kuona tatizo hilo, alitoa taarika kwa mafundi ambao walirekebisha tatizo na ndege hiyo sasa ipo kazini kama kawaida"

Naye kaimu wa Uwanja wa ndege wa Mwanza David Motovolwa alikiri kuwepo kwa tatizo hilo huku akidai kwamba ndege hiyo ilishindwa kuruka kutokana na hitilafu kwenye injini. 

ZAIDI sikiliza Jembe Fm 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.