ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, January 4, 2017

MSAKO WA WEZI WA UMEME SASA WAHAMIA JIJINI MWANZA. MMOJA ANASWA.


Shirika la umeme nchini(TANESCO) mkoa wa Mwanza limetakiwa kuimarisha ukaguzi wa mita ambazo hazilipiwi umeme ili kubaini watu wanaojihusha na wizi wa nishati ya umeme kwa lengo la kudhibiti vitendo hivyo ambavyo vimeshamiri jijini  mwanza.

Msako dhidi ya wezi wa nishati ya umeme ukiwa umebisha hodi katika nyumba moja ya makazi na biashara iliyoko mtaa wa rufiji jijini mwanza.

Msako umefanyika kwenye nyumba moja mkoani hapa baada ya mmiliki wake Greshen Magana kutoa taarifa kwa maafisa wa shirika la umeme nchini (TANESCO) juu ya kuwepo kwa wizi wa umeme unaofanywa na mtu aliyemkabidhi kuwa msimamizi wa  nyumba yake iliyo na makazi pamoja na biashara iliyoko eneo la rufiji jijini Mwanza.

Lakini Magana amewezaje kubaini wizi huo ilhali haishi kwenye nyumba hiyo?na vipi juu ya Matokeo ya ukaguzi ulioongozwa na Afisa usalama wa TANESCO mkoa Mwanza John Chilale...! BOFYA PLAY KUSIKILIZA TAARIFA HII. 

Wizi wa umeme kwenye nyumba hiyo ya makazi na biashara iliyoko eneo la rufiji jijini mwanza unakadiriwa kulisababishia shirika la Umeme TANESCO makadirio ya hasara ya zaidi ya shilingi milllioni tatu tangu februari mwaka jana.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.