ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 21, 2017

MRADI WA LVEMP2 SASA KUJA NA MBINU KUBWA ZA KUPAMBANA NA UCHAFUZI WA MAZINGIRA ZIWA VICTORIA.

NA ANNASTAZIA MAGINGA,
GSENGO BLOG 
Mwanza

KAMATI ya Bunge ya kudumu ya viwanda ,Biashara na Uwekezaji imewataka wataalamu wanaosimamia uhifadhi wa mazingira ziwa Victoria kwa awamu ya pili (LVEMPII) kuwa na mradi mkubwa utakao zuia uchafuzi katika ziwa hilo.

Hatua hiyo imekuja baada ya muwaslisha mradi ,mratibu wa LVEMPII Omary Myanza kueleza miradi inayotekelezwa na mradi huo katika kuondoa uchafuzi katika ziwa Victoria kupitia jamii.

Akizungumza kwenye kikao hicho Mwenyekiti wa kamati hiyo Dkt.Dalali Kafumu amesema kuwa mradi huo hauna mradi endelevu  utakaosaidia kukusanya na kuzuia uchafuzi na kulinda mazingira ya ziwa Victoria kwani iliyopo ni midogo midogo ambayo itakufa baada ya mradi kuisha muda wake.

“Kukiwa na mradi mkubwa utasaidia kwa sababu mradi huu unaisha Disemba 31mwaka huu na kama unaisha ina maana hata hii midogo midogo mnayowezesha wananchi pia itakufa kutokana na mradi utakuwa umekufa”amesema Kafumu.

Aidha awali akiwasilisha mradi huo mbele ya kamati hiyo mratibu Myanza amesema mradi wa LVEMP II umeanza  2009 sept na kutarajiwa kukamirika disemba 31 mwaka huu  huku ukiwa hadi sasa miradi 341 ikiwa imekwisha wanaufaisha wananchi.

“Miradi 203 imekamilika kwa 100%, 90 imekamirika zaidia ya 50% na 48% iko chini ya 50% kukamilika  miradi inayofadhiliwa na bank ya dunia kwa dolla milioni 42.5  za kimarekani na nchi yetu ilitoa dolla milioni 3  na kutekelezwa na nchi tano za Afrika mashariki”amesema Myanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.