ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 19, 2017

JPM AWAPANGIA VITUO MABALOZI WATANO.



Rais John Magufuli

Dar es Salaam. Rais  John Magufuli, leo (Alhamisi) amefanya uteuzi wa mabalozi watano watakaowakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi imesema mabalozi hao wataapishwa kesho (Ijumaa) Ikulu jijini hapa.
Mabalozi hao ni Emmanuel John Nchimbi ambaye ameteuliwa kuiwakilisha Tanzania Brazil, Mbelwa Brighton Kairuki ameteuliwa kuiwakilisha Tanzania, China, George Kahema Madafa ameteuliwa kuiwakilisha Tanzania Rome , Italy.
Fatma Rajab ameteuliwa kuiwakilisha Tanzania Doha, Qatar, Profesa  Elizabeth Kiondo ameteuliwa kuiwakilisha Tanzania Uturuki,  James Alex Msekela ameteuliwa kuiwakilisha Tanzania Geneva, Umoja wa Mataifa.
Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua Muhidin Mboweto kuwa balozi.
Tarehe ya kuapishwa na kituo cha kazi cha  Mboweto vitatangazwa baadaye.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.