ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, January 22, 2017

VIDEO ARSENAL YAIBAMIZA BURNLEY MABAO 2-1


Alexis Sanchez aliifungia Arsenal bao la pili dakika ya 98 kwa njia ya Penalti na kuiweza kuwashinda Burnley mabao 2-1 nyumbani mwa Arsenal huko Emirates.

Baada ya meneja wa Arsenal Arsene Wenger kutimuliwa uwanjani kwa kulalamikia uamuzi wa refa, kosa la Ben Mee la kumpiga kiatu Laurent Koscielny, lilisabaisha Burnley kuadhibiwa na Arsenal kupewa Penalti.
Alexis Sanchez aliifungia Arsenal bao la pili

Arsenal walikuwa wameitawala mechi hadi pale Granit Xhaka alipotimuliwa baada ya kumchezea visivyo Steven Defour, hali iliyosababisha Burnley kunufaika.

Ushindi wa mara tano wa Arsenal katika uga wao wa Emirates, unawapandisha jedwali juu na Liverpool na Tottenham, ambao wote walipoteza pointi siku ya Jumamosi na kupunguza mwaya kati yao na Chelsea hadi pointi tano.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.