ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, November 12, 2016

CHANGAMOTO MOJA TU KUITWA WAKISASA ILE YA UKWELI UKWELI.

Neema imekaribia kwa wapenda soka wa jiji la Mwanza na Watanzania wote baada ya nyasi kuanza kutandikwa kwenye Uwanja wa Nyamagana.

Uwanja wa Nyamagana uko katikati ya jiji la Mwanza na wakati fulani nusura serikali iutoe, eti ijengwe hoteli ya kitalii.

Yote 9 kumi uwanja bado unachangamoto nyinginezo mwanawane... zaidi cheki VIDEO HAPO JUU kwa hisani ya Gsengo Tv.
Tembea nami Gsengo toka Mwanza Tanzania.

Kona na muonekano taswira ya uwanja.

Engo moja pande za mashariki ya uwanja.

Mchanga mweusi kwenye mifuko ndiyo itakuwa hitimisho la mwisho baada ya mchanga awamu zote kukamilika unynyizaji.

Pembe ya uwanja wa Nyamagana.

Kona ya Kaskazini mashariki.

Juu ya nyasi na zoom.

Kona ya goli la kusini.

Toka engo.

Paleeee kati.

Japo kwa juu karibu kiduchu Goli hadi goli

Kutoka juu na muonekano uwanja wa Nyamagana Mwanza.

MHE. MONGELA AIKOMALIA VITA DHIDI YA UVUVI HARAMU UKEREWE NA ZIWA VICTORIA KWA UJUMLA.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza aiagiza serikali wilayani  Ukerewe yatakiwa kupambana vikali kukomesha uvuvi haramu mkoani humo.

TATHIMINI UNGWE YA KWANZA LIGI KUU SOKA TANZANIA BARA 2016-2017

VIDEO KILICHOJIRI japo uduchu ndani ya kipindi cha KIPENGA

Time yako asubuhi hii kukutana nasi kispoti zaidi #KIPENGA ndicho kipindi ukiwa na @jumaayoo @elikanamathias featuring wachambuzi wa siku ya leo ni @salehjembe na wakali wengine. Majogoli kuhusishwa kama kawa safari hii tunatua pale mjini Shinyanga na kisha tunapaa hadi jijini Dar es Salaam ndani ya Club ya Azam FC suala la kukuza vipaji #VeePe!!?!! Tupate popote ulimwenguni kupitia Google play store kwa kusachi JEMBE Fm HD kisha sikiliza LIVE kupitia simu yako ya mkononi AU nenda kwenye TUNe in search JEMBE FM aksante kwa kutusikiliza. @djscopion

CHANZO/GAZETI LA CHAMPION 
...Nahodha wa Simba, Jonas Mkude, ameonyesha ukomavu kwa kusema licha ya timu yake kupoteza mechi mbili mfululizo, bado hawajakata tamaa na nia yao ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara iko palepale.

Simba ipo kileleni mwa ligi kuu ikiwa na pointi 35 lakini imepoteza mechi mbili mfululizo dhidi ya African Lyon (bao 1-0) na Prisons kwa mabao 2-1 kabla ya ligi hiyo kusimama.

Katika mechi 15 za ligi, Simba imeshinda 11, imetoka sare mbili na kufungwa mbili, Mkude amesema takwimu hizo haziwezi kuwatoa katika mbio za ubingwa msimu huu.

Kiungo huyo amesema kuwa, kupoteza mechi mbili ni sehemu ya mchezo lakini wameshabaini makosa yao waliyoyafanya na baada ya mapumziko watayafanyia kazi na kurudi tena katika moto wao.

“Tumefungwa kwa sababu huu ni mchezo ambao una matokeo matatu na tumepokea matokeo haya na hatuna budi kukazana kwenye mechi zijazo kuhakikisha kwamba hatupotezi kama ilivyotokea kwenye mechi hizi mbili za mwisho.


“Hatujakata tamaa kutokana na kufungwa kwani ndiyo kwanza vipigo vimetuamsha zaidi na tutajitahidi kupambana kwa kila hali katika mzunguko wa pili tufanye vizuri,” alisema Mkude.


Mwadui FC sasa ipo chini ya Khalid Mohammed ambaye ametamba timu yake kutisha katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara.

Mohammed amechukua nafasi ya Jamhuri Kihwelo 'Julio' ambaye 'alikimbizwa' na waamuzi wasiotenda haki.

Mohammed amesema wakati huu ambapo ligi imesimama, amewapa mapumziko mafupi vijana wake kisha watarejea kwa mazoezi makali kambini kwao na ana imani watafanya vizuri mzunguko wa pili.

Mwadui ipo katika nafasi ya 15 katika ligi ambayo si nzuri ikiwa na pointi 13 katika mechi 15 ilizocheza ambapo imeshinda tatu, imetoka sare nne na kufungwa mara nane.

Mohammed amesema kuwa: “Unajua siyo kila msimu timu inakuwa na matokeo mazuri, hii hali inaweza kuitokea timu yoyote ile, sasa tunaenda kujipanga.


“Katika kikosi kuna upungufu mdogo nimeubaini, hasa kwenye kiungo na ulinzi, tutakitumia kipindi kijacho cha usajili wa dirisha dogo kuimarisha kikosi, naamini mzunguko wa pili tutakuwa vizuri.”

ALIYEUA MTU CHUMBANI AKAMATWA NA POLISI.

JESHI la Polisi mkoani Manyara, limemkamata mhusika wa tukio la mauaji ya mtu aliyekutwa chumbani akiwa amekufa huku mwili wake ukiwa sakafuni pembeni ya kitanda katika mtaa wa Negamsi, kata ya Bagara, mkoani humo.
Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Oktoba 30, mwaka huu, saa nne asubuhi ambapo, Alex Charles (27), mkazi wa mtaa wa Negamsi katika kata ya Bagara, tarafa ya Babati alikutwa chumbani kwake amekufa.

Kamanda wa Polisi mkoani humo, Francis Massawe akizungumza na gazeti hili jana alisema, mtu huyo alikutwa ameuawa na watu wasiojulikana nyumbani kwake kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali katika paji lake la uso na kuvunjwa taya la upande wa kushoto na kusababisha kuvuja damu nyingi, hatimaye kupoteza maisha.

Alisema mtuhumiwa huyo ambaye jina limehifadhiwa kwa ajili ya upelelezi, anadaiwa alikuwa mtu wa karibu na familia ya marehemu na alikuwa akiishi nayo kwa muda mrefu, na alipohojiwa alikiri kuua na kwamba alifanya hivyo kwa kujitetea kutokana na kutaka kumlawiti.

Kamanda Massawe alieleza kuwa, mtuhumiwa huyo alikamatwa Novemba 8, mwaka huu, akiwa na mali alizoiba katika nyumba ya marehemu zikiwamo pasi ya umeme, deki, viatu na suruali ya jeans, sweta na koti moja la marehemu.

Vifaa hivyo vilitambuliwa na mke wa marehemu na muuaji huyo, ambapo mtuhumiwa huyo alikiri kuhusika na mauaji hayo peke yake na kisa ni kwamba alikuwa ametishwa na marehemu kuwa atamuua kwa mkuki na katika kujitetea ndipo akamwahi.

Mtuhumiwa huyo aliendelea kueleza kuwa Alex, alipokuwa naye chumbani kwake siku ya tukio, alitaka kumlawiti na walibishana naye kitambo, ndipo akamsukuma na kumbamiza ukutani na kupiga yowe.

Katika hatua nyingine, Kamanda Masawe alisema, Matayo Yohana (19) dereva bodaboda akiwa njiani alisimamishwa na mtu aliyejifanya abiria na ndipo watu wengine wanne walijitokeza na kuanza kumpiga na kumjeruhi mguu wa kushoto.

Alisema watu hao walipora pikipiki hiyo yenye namba za usajili MC 500 AYH aina ya King Lion, mali ya Joachim John, baada ya kuporwa, msako ulifanyika kwa kushirikiana na wananchi, ndipo watuhumiwa tatu walipatikana wakiwa na pikipiki nyingine mali ya Edmund Peter (40) yenye namba za usajili T814 CCM.

TASWIRA YA 'KIPENGA' ASUBUHI NDANI YA JEMBE FM

 Time yako asubuhi hii kukutana nasi kispoti zaidi #KIPENGA ndicho kipindi ukiwa na @jumaayoo @elikanamathias featuring wachambuzi wa siku ya leo ni @salehjembe na wakali wengine. Majogoli kuhusishwa kama kawa safari hii tunatua pale mjini Shinyanga na kisha tunapaa hadi jijini Dar es Salaam ndani ya Club ya Azam FC suala la kukuza vipaji #VeePe!!?!! Tupate popote ulimwenguni kupitia Google play store kwa kusachi JEMBE Fm HD kisha sikiliza LIVE kupitia simu yako ya mkononi AU nenda kwenye TUNe in search JEMBE FM aksante kwa kutusikiliza. @djscopion
BOFYA HAPA KUSIKIA 'MAJOGOLI'

Wachambuzi wa michezo ndani ya Studio za Jembe Fm Radio Mwanza wakiwa katika meza ya majadiliano subuhi hii.


Mkurugenzi wa Gazeti la The Champion ambaye pia ni mhariri wa michezo wa Gazeti hilo Saleh Jembe (kushoto) akiwa na mchambuzi wa michezo Emmanuel Mtindi wa Jembe Fm.


Mkurugenzi wa Gazeti la The Champion ambaye pia ni mhariri wa michezo wa Gazeti hilo Saleh Jembe (kushoto) akiwa na mchambuzi wa michezo Emmanuel Mtindi wa Jembe Fm.


Debe na Jembe.


Debe na Jembe two.
@salehjembe & @gsengo


#DebeNAjembe = "Linda kibarua chako, linda kazi yako, linda ajira yako, weka ubunifu kila iitwapo leo, waite wateja wako kwa ubunifu na ukarimu so piga Debe kwa style na kweli utafanikiwa" @salehjembe


Timu 'KIPENGA' ya leo 

Friday, November 11, 2016

MAMA JANETH MAGUFULI ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI

Rais Magufuli alipomtembelea mkewe siku ya jana katika hospitali ya Taifa Muhimbili
CHANZO BBC SWAHILI.

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli aliyekuwa amelazwa katika wodi ya Sewahaji ya Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam ameruhusiwa na kurejea nyumbani leo baada ya afya yake kuimarika.
Kabla ya kuondoka katika wodi ya Sewahaji alikokuwa amelazwa Mama Janeth Magufuli amewashukuru Madaktari na Wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu mazuri aliyoyapata na pia amewashukuru Watanzania wote kwa kumuombea afya njema.

"Namshukuru sana Mungu kwamba afya yangu imeimarika, pia napenda kuwashukuru Madaktari na Wauguzi, nimepata huduma nzuri sana maana siku nilipoletwa hapa nilikuwa sina fahamu na hali yangu ilikuwa mbaya lakini mmenipigania na leo narudi nyumbani nikiwa na afya imara.

"Naomba pia niwashukuru Watanzania wote kwa kuniombea, nawahakikishie kuwa sasa nipo vizuri na madaktari wameniruhusu nirudi nyumbani ambako nitamalizia matibabu yangu" amesema Mama Janeth Magufuli.

Mama Janeth Magufuli alilazwa hospitalini hapo tangu Juzi tarehe 09 Novemba, 2016 baada ya kuugua ghafla na kupoteza fahamu.

VIDEO YA MAGOLI MCHEZO WA BRAZIL V/S ARGENTINA 3-0 11/11/2016

Video ya Mchezo wa Brazil dhidi ya Argentina






AIRTEL YAZINDUA VIFURUSHI VYA KIMATAIFA NDANI NA NJE YA NCHI.

Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando (katikati), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya vifurushi vya kimataifa ndani na nje ya nchi, vitakavyomwezesha mteja kupiga simu kwenda nchi zaidi ya 20 kwa gharama nafuu. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Biashara za Kimataifa wa Airtel, Prisca Tembo na Meneja wa kitengo hicho, Alice Paulsen. 
Mkuu wa Kitengo cha Biashara za Kimataifa wa Airtel, Prisca Tembo (kulia), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya vifurushi vya kimataifa ndani na nje ya nchi, vitakavyomwezesha mteja kupiga simu kwenda nchi zaidi ya 20 kwa gharama nafuu. Katikati  ni Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando na Meneja wa kitengo hicho, Alice Paulsen. 

Airtel yazindua vifurushi vya kimataifa ndani na nje ya nchi

·         sasa wateja kununua vifurushi vya kupiga simu za kimataifa kwenda nchi zaidi ya 20
·         wateja kujitengenezea vifurushi vya intaneti pindi wanapotembelea nchi  ambazo Airtel inazofanya biashara barani Afrika

Dar es Salaam, Alhamis 10 Novemba 2016, Airtel Tanzania leo imetangaza ofa kabambe itakayowawezesha wateja wake nchi nzima kununua vifurushi wavipendavyo na kupiga simu kwenda nchi zaidi ya nchi 20 kwa gharama nafuu 

Pamoja na vifurushi vya kupiga simu nje ya nchi , Airtel pia imezindua vifurushi vya intaneti vya roaming  mahususi kwa wateja wanaotembelea nje ya nchi vijulikanavyo kama “Safari Internet Roaming” vitakavyowapatia uhuru wateja wake  kupanga matumizi yao ya intaneti pindi wanapotembelea nchi ambazo Airtel inafanya biashara zake barani Afrika. Nchi hizo ni pamoja na Burkina Faso, Chad, Congo Brazzaville, DRC, Kenya, Gabon, Ghana, Madagascar, Malawi, Niger, Nigeria, Rwanda, Seychelles, Sierra Leone, Uganda na Zambia.

Akitangaza ofa hiyo Meneja Biashara za Kimataifa wa Airtel, Prisca Tembo alisema” Tunayofuraha kutangaza ofa nyingine kabambe itakayowapa wateja wetu uhuru katika mahitaji yao ya mawasiliano na kuwawezesha kuwasiliana na familia, marafiki na wafanyabiashara wenzao barani Afrika na kimatifa kwa urahisi zaidi.  Ofa yetu ya kupiga simu nje ya nchi inamhakikishia mteja thamani ya pesa yake na urahisi katika huduma za mawasiliano na kupata faida lukuki za kujiunga na timu SIBANDUKI.  Vifurushi vyetu vya kupiga simu nje ya nchi zinapatikana kwa siku, wiki au mwezi kwa kupiga  *149*13# au kupitia Airtel Money kwa kupiga *150*60#.  Mteja anaweza kujinunulia kifurushi akipendacho na kupiga simu kwenda zaidi ya nchi 20 kwa gharama nafuu”

Tembo aliongeza kwa kusema “vifurushi vipya vya intaneti vya roaming yaani wateja wanaotembelea nje ya nchi zinaenda sambamba na dhamira yetu ya kuendelea kutoa huduma za mawasiliano za kibunifu, gharama nafuu na zenye ubora kwa watanzania zinazovuka zaidi ya mipaka ya nchi. Idadi ya watanzania wanaosafiri nje ya nchi kibiashara na safari za kawaida inakuwa kwa kasi, vifurushi vyetu vipya vya nje ya nchi vitawawezesha kupanga matumizi yao na kuwaepusha na ankra kubwa na kuwahakikishia mawasiliano mahali popote waliko”

Ofa hizi za kupiga simu nje ya nchi na vifurushi vya intaneti nje ya nchi ni kwa wateja wa malipo ya awali yaani ”prepaid”  nchi nzima

Nchi ambazo mteja anaweza kupiga simu nje ya nchi kwa kununua vifurushi vya kimataifa ni pamoja na Zambia, Malawi, DRC, South Africa, India, China, USA, Canada, Uganda, Rwanda, Kenya, Oman, UAE, Saudi Arabia, Yemen, Lebanon, Pakistan, Qatar, Uingereza, Itali na Ujerumani.

RAIS MAGUFULI AKITOA SALAMU ZA MWISHO.

Rais John Magufuli akipita kutoa heshima ya mwisho kuaga mwili wa marehemu Samuel Sitta katika viwanja vya Karimjee.

WAZIRI ANGELLAH KAIRUKI AKISOMA SALAM ZA SERIKALI.

Waziri wa nchi ofisi ya Rais Angellah Kairuki akitoa salamu za serikali kwa ndugu wa marehemu Samuel Sitta viwanja vya Karimjee Dar es Salaam.

Thursday, November 10, 2016

MZIGO WA MAJI BAHARI WATUA MWANZA.

Chukua namba hizo.

MADAKTARI MABINGWA WA UPASUAJI TOKA NCHINI INDIA WAANZA HUDUMA BURE YA KUTIBU NA UPASUAJI WAGONJWA WA MOYO KATIKA HOSPITALI YA BUGANDO JIJINI MWANZA.

Mkuu wa Kitengo cha upasuaji wa Kifua na Moyo BMC, Prof. William Mahalu akizungumza (kulia) kwenye mkutano na waandishi wa habari wakati wa kuwakaribisha madaktari bingwa wa upasuaji wa Moyo kutoka Madras Medical Mission, Chennai, India katika hafla iliyofanyika kwenye Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza, pembeni yake ni Rais wa Jumuiya ya Shia Imami Islaili Muslims, Kanda ya Magharibi Bw. Altaf Hirani.
 Gharama za upasuaji wa Moyo ni kubwa si chini ya shilingi Millioni 6 za Tanzania. Kwa wagonjwa hawa tunashukuru Wizara ya Afya,Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando Medical Centre (BMC) lakini shukurani nyingi ziende MMI ambao wamenunua vifaa vingi ba ambavyo watatuachia hapa, ili tuendelee naupasuaji huu.
Sehemu ya madaktari wageni toka nchini India wakiwa kwenye mkutano na waandishi wa habari wakati wa kuwakaribisha madaktari hao mabingwa wa upasuaji wa Moyo kutoka Madras Medical Mission, Chennai, India katika hafla iliyofanyika kwenye Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza. Wa pili kutoka kushoto ni Bingwa wa Moyo kwa watoto daktari mzalendo aliyerejea nchini Dr. Glory Joseph ambaye ndiye aliyekuwa akisimamia zoezi hilo. 


Kwa mujibu wa Rais wa Jumuiya ya Shia Imami Islaili Muslims, Kanda ya Magharibi Bw. Altaf Hirani (katikati) amesema kuwa kila mwaka Hospitali ya Aga Khan inatumia shilingi za Kitanzania bilioni 2 kuwahudumia wagonjwa bila malipo yoyote ambapo hadi sasa zaidi ya wagonjwa 600 wamefanyiwa upasuaji wa moyo.

Watanzania madaktari 10 walipelekwa nchi za nje kupata mafunzo zaidi. Aidha Wakfu wa Afya wa Aga Khan umewekeza shilingi za kitanzania bilioni 167 katika ujenzi wa Hospitali ya kisasa ya kutoa mafunzo ya udaktari ambayo tayari imeanza kujengwa. 

Pia kujengwa vituo 35 vya afya vitajengwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini, vitano vikiwa katika mkoa wa Mwanza.
BOFYA PLAY KUSIKILIZA.
Bingwa wa Moyo kwa watoto daktari mzalendo aliyerejea nchini Dr. Glory Joseph ambaye ndiye aliyekuwa akisimamia zoezi hilo. Nini sababu za watoto kuzaliwa na maradhi ya moyo na vipi kuhusu dalili, Hapa anafunguka zaidi. BOFYA KUSIKILIZA.


 Timu ya madaktari mabingwa wapatao 14 wako kwenye mpango huu wa kupima na kutibu kwa dawa na timu kamili ya kutibu kwa kupasua ikitegemea katika muda wa siku 6 yaani kuanzia tarehe 7 hadi 12 mwezi November kupasua waonjwa 10 wakiwemo wakubwa wanne (4) na watoto 6.

Wakati huo huo mabingwa hao wa maradhi ya moyo wataendelea kupima na kuchunguza watoto wenye magonjwa hayo ambapo mpaka sasa wameshapima watoto 50.
Sehemu ya akinamama ambao wamejitokeza kupima afya za watoto wao na hapa wakisubiri matibabu mara baada ya watoto wao kugundulika kuwa na matatizo kwenye afya ya moyo.


Ni moja ya akinamama ambao watoto wao wanasubiri kufanyiwa oparesheni katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza.


"Nasubiri kuiona siku mpya kwa mwanangu, siku itakayo kuwa mwanzo wa maisha yake yaliyo salama" 
BOFYA KUSIKILIZA NINI WALICHOSEMA AKINAMAMA HAWA

Mzazi huyo anakesha hapa kusubiri upasuaji.


Rais wa Jumuiya ya Shia Imami Islaili Muslims, Kanda ya Magharibi Bw. Altaf Hirani akimjulia hali mtoto David Rashid anayesumbuliwa na maradhi ya moyo akisubiri upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza.


Ndani ya chumba cha Upasuaji Oparesheni inaendelea chini ya madaktari mabingwa wa upasuaji wa Moyo kutoka Madras Medical Mission, Chennai nchini India na madaktari wakizalendo kutoka nchini Tanzania.


Ndani ya chumba cha Upasuaji na hapa Oparesheni inaendelea chini ya madaktari mabingwa wa upasuaji wa Moyo kutoka Madras Medical Mission, Chennai nchini India na madaktari wakizalendo kutoka nchini Tanzania.


Ndani ya chumba cha Upasuaji Oparesheni madaktari wasaidizi.


Kwa umakini zaidi ndani ya chumba cha Upasuaji hapa Oparesheni inaendelea chini ya madaktari mabingwa wa upasuaji wa Moyo kutoka Madras Medical Mission, Chennai nchini India na madaktari wakizalendo kutoka nchini Tanzania.


Mmoja ya wanahabari wetu Zephania Mandia kikazi zaidi.


G. Sengo ndani ya chumba cha Upasuaji, Oparesheni inaendelea chini ya madaktari mabingwa wa upasuaji wa Moyo kutoka Madras Medical Mission, Chennai nchini India na madaktari wakizalendo kutoka nchini Tanzania.

PLUIJM AWAAGA VYEMA YANGA, AMKARIBISHA LWANDAMINA KWA USHINDI WA 2-1.

KOCHA Mholanzi, Hans van der Pluijm leo amewaaga vizuri wana Yanga baada ya kuiongoza timu hiyo kushinda 2-1 katika m chezo wa mwisho wa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Ushindi huo unaifanya Yanga imalize na pointi 33 nyuma ya Simba SC yenye pointi 35 kileleni baada ya mechi 15 za mzunguko wa kwanza.

Sifa zimuendee kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima kwa ushindi wa leo kutokana na kuseti bao la kwanza na kufunga bao la pili.

Lakini Yanga ililazimika kutoka nyuma baada ya Ruvu kutangulia kwa bao la Abrahman Mussa aliyemalizia krosi ya Fully Zulu Maganga dakika ya saba na kumtungua kipa Benno Kakolanya.

Hata hivyo Nahodha wa Yanga leo, Niyonzima akamtoka kwa chenga maridadi kabisa beki Mau Boffu kabla ya kutia krosi iliyounganishwa nyavuni na winga Simon Msuva kuisawazishia Yanga dakika ya 32.

Refa Mathew Akrama wa Mwanza alisindikizwa na Polisi huku akitolewa maneno ya ukali na kocha wa Yanga, Pluijm baada ya kupuliza filimbi ya kukamilisha dakika 45 za kipindi cha kwanza.

Na haikuwa ajabu refa huyo alipomtoa kwenye benchi Pluijm kabla ya kuanza kipindi cha pili.

Niyonzima aliifungia bao la ushindi Yanga dakika ya 56 kwa shuti la mbali kufuatia mpira uliorudi baada ya shambulizi kali langoni mwa Ruvu.

Yanga wakatulia na kuanza kucheza kwa kupasiana ili kuumiliki mpira kwa lengo la kuwapunguza kasi Ruvu wafanikiwe kuulinda ushindi wao.

Pluijm anaondoka Yanga kumpisha Mzambia, George Lwandamina atakayeanza kazi mzunguko wa pili wa Ligi Kuu.

Na Pluijm anaondoka baada ya kuiongoza Yanga kwa awamu mbili tangu mwaka 2014 akicheza jumla ya mechi 128, akishinda 80, kufungwa 23 na sare 25.

Mwaka 2014 aliiongoza Yanga katika mechi 19, akishinda 11, kufungwa mbili na sare sita kabla ya kuondoka kwenda Al Shoalah FC ya Saudi ya Arabia na nafasi yake ikachukuliwa na Mbrazil, Marcio Maximo.

Maximo alifanya kazi kwa nusu msimu kabla ya Pluijm kurejeshwa Januari mwaka jana.  Saudi Arabia ambako alikwenda na aliyekuwa Msaidizi wake, Yanga SC, Charles Boniface Mkwasa – Pluijm  aliondoka baada ya kutofautiana na uongozi wa timu uliotaka kumsajilia wachezaji asiowataka.

Na kuanzia Januari mwaka jana, Pluijm ameiongoza Yanga katika mechi 109, akishinda 69, sare 19 na kufungwa 21.

Na Pluijm anaiachia Yanga mataji mawili ya Ligi Kuu, mawili ya Ngao ya Jamii na moja Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Kombe la Azam Sports Federation Cup (ASFC).

Katika mchezo wa leo, Pluijm hakuketi kwenye benchi la Yanga, bali alichukua kiti na kuketi pembeni ya benchi hilo kuashiria kwamba anaondoka.

Kikosi cha Yanga leo kilikuwa; Beno Kakolanya, Hassan Kessy, Mwinyi Hajji, Kevin Yondan, Andrew Vincent, Thabani Kamusoko, Simoni Msuva, Haruna Niyonzima, Donald Ngoma/Matheo Anthony dk86, Amissi Tambwe na Obrey Chirwa/Juma Mahadhi dk60.

Ruvu Shooting; Abdallah Rashid, Said Madega, Mau Ali Bofu/Yussuf Nguya dk79, Renatus Kisase, Shaibu Nayopa, Jabir Aziz, Abrahman Mussa, Zubeiry Dabi/Raphael Kyala dk60, Issa Kanduru, Fully Maganga/Said Diliunga dk70 na Chande Magoja.

KAKAKUONA AMEONEKANA KWENYE MIGODI YA MERERANI.


Mnyama adhimu anayetumika kutabiri matukio mbalimbali katika jamii kakakuona ameonekana kwenye migodi ya madini ya Tanzanite Mererani wilayani Simanjiro huku wachimbaji wakionekana kumgombania kumgusa wakitaka baraka na kudai neema ya madini imekaribia kwenye migodi hiyo.


Katika eneo la mchimbaji mdogo anayejulikana kwa jina la Dunia umati wa wachimbaji wadogo wametiririka kutaka kumgusa mnyama huyo wakidai kuchukuwa baraka tofauti na maeneo mengine ambayo humwekea vifaa vingi kuchagua lakini wachimbaji hao wakimuwekea fedha pekee.

Mlinzi wa mgodi huo anaeleza alivyomuona mnyama huyo. BOFYA PLAY KUSIKILIZA.


KAMA UNATAKA KUMJUA ZAIDI.

Kuna aina nane za kakakuona duniani.

Aina hizo nane za kakakuona zimetoka katika familia inayofahamika kama manidae. Aina hizo za kakakuona zipo duniani kwa zaidi ya miaka 80 milioni ya mabadiliko yao.

Kati ya hizo, aina nne za kakakuona zinapatikana katika Bara la Ulaya na wengine barani Afrika. Hawa wanafahamika kwa majina ya tree kakauona, giant kakakuona, cape kakakuona na kakakuona wenye mkia mrefu.

Ulimi mrefu kuliko mwili wake

Kakakuona ana ulimi wenye urefu unaozidi mwili wake. Akiurefusha kwa kuutoa nje ya kinywa unafikia urefu wa sentimita 40.

Ulimi huo ambao pia unanata, huutumia kwa ajili ya kukusanya wadudu ambao ndiyo mlo wake wa pekee, hana mwingine zaidi ya huo kutokana na kukosa meno.

Ndiye mnyama pekee duniani ambaye mwili wake wote umefunikwa na magamba makubwa

Magamba yanayofunika mwili wa mnyama huyo ni makubwa kuliko ya viumbe wengine. Magamba hayo kitaalamu yameundwa na kitu ninachoitwa ‘keratin’, ambayo yanafanana na yale yanayounda kucha za binadamu.

Asilimia 20 ya uzito wa mwili wa mnyama huyo unatokana na magamba.

Kakakuona hutumia magamba hayo kama silaha ya kujilinda dhidi ya maadui.

Maana ya jina kakakuona

Maana ya jina hilo ilianzia nchini Malaysia, Indonesia na Brunei likimaanisha kitu kinachojikunja. Kakakuona hupenda kujikunja kama mpira. Hiyo ikiwa kama mbinu anayotumia kujilinda dhidi ya maadui.

Licha ya kuwa hutumia mbinu hiyo kujilinda, lakini anapojikunja ndiyo inakuwa rahisi kwa watu kumkamata na kumbeba.

Huishi juu ya miti na katika mashimo

Baadhi ya kakakuona huishi juu ya miti, wengine hujichimbia ardhini na kuishi ndani ya mashimo.

Wengi wanaoishi juu ya miti ni wale wenye mikia mirefu wanaopatikana barani Afrika. Wengine huchimba mashimo marefu ardhini na kuishi humo ili wasikutane na binadamu.

Si rahisi kushambuliwa na wanyama wengine

Ukiachilia mbali adui yao mkubwa ambaye ni binadamu, adui wengine wa wanyama huyo ni jamii ya chui na simba.

Hata hivyo, maadui hao hushindwa kuwashambulia kakakuona kutokana na namna wanavyojilinda kwa kujikunja na jinsi mwili wao ulivyo na magamba. Kutokana na hali, hiyo inakuwa vigumu kwa simba au wanyama wengine kuwashambulia kwa kuwala.

Hakuna anayefahamu idadi ya miaka anayoishi

Inakadiriwa kuwa mnyama huyo huishi kwa kipindi cha miaka 20 akiwa katika pori. Lakini hiyo ilikuwa inafahamika zamani kipindi ambacho mnyama huyo alikuwa anaonekana tofauti na sasa.

Hata hivyo, kutokana na aina ya maisha ya wanayoishi, inasemekana kuwa wanaweza wasiishi miaka mingi, licha ya kuwa bado haifahamiki kwa sasa, inawezekana wakaishi kwa miaka 20.

Hutema sumu kali mithili ya tindikali

Kakakuona akiona adui hujilinda kwa kujikunja, lakini akiona hali inakuwa mbaya zaidi, hutema sumu kali mithili ya tindikali inayoweza kumdhuru adui.

Pia, wakati mwingine hunyoosha mkia wake na kuuzungisha na kumkata adui aliyekaribu yake.

Mamilioni wameuawa na kuuzwa katika miaka 10 iliyopita

Inakadiriwa kuwa kakakuona 100,000 hukamatwa kila mwaka barani Afrika na Ulaya na kuuzwa. China na Vietnam ndizo nchi maarufu ambazo nyama na magamba yake huuzwa.

Kutokana na hilo, Shirika la Umoja wa Mataifa la Hifadhi za Asili (IUCN) limemweka kakakuona kwenye orodha ya wanyama walioko kwenye hatari ya kutoweka duniani.

Hawaoni vizuri

Ni aina moja katika ya nane za kakakuona wenye uwezo wa kuona vizuri hasa muda wa mchana. Hawa ni wale wanaopatikana barani Afrika.

Wengine hawana uwezo wa kuona vizuri kutokana na kuwa na macho madogo.

Wana uwezo mkubwa wa kunusa na kusikia

Licha ya wengine kuwa na macho madogo na kushindwa kuona vizuri, kakakuona ni mnyama mwenye uwezo mkubwa wa kusikia sauti yoyote kwa haraka kwa sababu masikio yake yameinuka. Pia, ana uwezo mkubwa wa kunusa harufu yoyote.

Ni vigumu kujamiiana

Tofauti ilivyo kwa baadhi ya wanyamaa, upande wa kakakuona tendo kujamiiana ni gumu kutokana na tofauti za kimwili kati ya jike na dume. Mwili wa kakakuona dume una uzito mkubwa zaidi ya asilimia 50 ukilinganishwa na jike.

Mbali na hivyo, hawana msimu maalumu kukutana na kujamiiana, tofauti na ilivyo kwa wanyama wengine.

Uhusiano na wanyama wengine

Imezoeleka kuwa, mnyama huyo huwa karibu na wanyama wengine wa jamii yao, kwa maana ya wale wanaokula wadudu.

Hata hivyo, hivi karibuni wanasayansi wamebainisha kuwa wamekuwa karibu na wanyama kutoka jamii nyingine kama wale wanaokula nyama.