ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 3, 2016

SHILINGI MILIONI 225 ZAHUDUMIA WANAFUNZI HEWA KAHAMA.

Kahama.
Wanafunzi hewa waliobainika wilayani Kahama, wameisababishia hasara Serikali ya Sh225 milioni kwa kipindi cha miezi minane kuanzia Januari hadi Agosti.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Fadhili Nkulu alisema kamati maalumu aliyounda imebaini uwapo wa wanafunzi hewa 29,000, ambao wamekuwa wakiisababishia hasara Serikali kila mwezi.

“Serikali ya Awamu ya Tano tangu iingie madarakani imekuwa ikituma fedha kila shule kwenye mpango wa elimu bure, lakini maofisa elimu, waratibu kata, walimu wakuu wa shule za msingi na sekondari wamebuni mbinu za kula fedha hizo kwa kuweka wanafunzi hewa kwenye shule zao,” alisema Nkulu.

Alitoa siku tatu kwa kila halmashauri kuwasilisha takwimu sahihi za wanafunzi ambazo zitalingana na idadi aliyonayo iliyopatikana baada ya kamati ya uchunguzi.

KAULI YA KOCHA WA YANGA BAADA YA NGASSA KUVUNJA MKATABA SOUTH

Mrisho Ngassa (kushoto) akimtoka mchezaji wa timu pinzani katika moja ya mechi za Ligi Kuu ya ABSA Afrika Kusini
 Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm, amempa ugumu aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Free States ya Afrika Kusini, Mrisho Ngassa kurejea kuichezea timu hiyo.

Hiyo, ni siku moja tangu taarifa za kiungo huyo kusitisha mkataba wake wa kuichezea Free States kwa makubaliano huku tetesi zikienea kuwa nyota huyo atarejea kucheza Yanga kwenye usajili wa dirisha dogo la Ligi Kuu Bara msimu huu.

Ngassa, alisitisha mkataba wa kuendelea kukipiga Sauz kwa kile alichodai kuwa timu hiyo haina malengo ya kutwaa ubingwa zaidi kushiriki kwenye ligi kuu.


Pluijm alisema kwenye kikosi chake hahitaji kiungo mshambuliaji kwani tayari anao wanne, tena vijana wenye uwezo mkubwa wa kuendana na kasi yake.

Pluijm aliwataja viungo hao washambuliaji kuwa ni Mzambia, Obrey Chirwa, Juma Mahadhi, Simon Msuva na Deus Kaseke ambao anaamini bado wana uwezo mkubwa wa kuichezea timu hiyo kwa muda mrefu kutokana na umri wao.

Aliongeza kuwa, haoni sababu ya kujaza viungo wengi washambuliaji kwenye kikosi chake kutokana na kutokuwa na tatizo katika nafasi hiyo.

“Nimepata taarifa za Ngassa kusitisha mkataba wake wa kuichezea Free States, labda nikwambie tu, ni ngumu kwangu kusajili kiungo mshambuliaji katika kikosi changu kwa hivi sasa, kwani tayari ninao wanne ambao ni vijana wenye uwezo mkubwa wa kucheza.


“Wachezaji wanaocheza nafasi hiyo (ya Ngassa) ni Chirwa, Mahadhi, Kaseke na Msuva, wote ni wazuri. Tofauti na kasi yao ya kushambulia, pia wana uwezo wa kufunga mabao, ni aina ya uchezaji aliyonayo Ngassa,” alisema Pluijm.

RAIS DKT MAGUFULI ATOA POLE NYUMBANI KWA MAREHEMU MZEE ABOUD JUMBE MWINYI, AWEKA SHADA LA MAUA KABURINI

jz21na 22: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitambulishwa kwa Bw. Mustapha Aboud Jumbe na Rajabu Aboud Jumbe alipokwenda kutoa mkono wa pole kwa familia ya Rais wa awamu ya Pili ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi nyumbani kwao Migombani Zanzibar mjini leo Septemba 3, 2016

j23, 24 na 25: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimu wanafamilia  alipokwenda kutoa mkono wa pole nyumbani kwa  Rais wa awamu ya Pili ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi nyumbani kwao Migombani Zanzibar mjini leo Septemba 3, 2016

j26: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka sahihi kitabu cha maombolezo  alipokwenda kutoa mkono wa pole nyumbani kwa  Rais wa awamu ya Pili ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi nyumbani kwao Migombani Zanzibar mjini leo Septemba  3, 2016

j27: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akielekezwa jambo na Rajabu Aboud Jumbe alipokwenda kutoa mkono wa pole nyumbani kwa  Rais wa awamu ya Pili ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi nyumbani kwao Migombani Zanzibar mjini leo Septemba 3, 2016. Nyuma yao ni Mama Janeth Magufuli na wanafamilia wa Mzee Jumbe.

j28 na j29: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka shada la maua kaburini na kutoa heshima zake alipokwenda kutoa mkono wa pole nyumbani kwa  Rais wa awamu ya Pili ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi  Migombani Zanzibar mjini leo Septemba 3, 2016.

jz30: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na ujumbe wake wakishiriki dua alipokwenda kutoa mkono wa pole nyumbani kwa  Rais wa awamu ya Pili ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi nyumbani kwao Migombani Zanzibar mjini leo Septemba 3, 2016


jz31:Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiaga baada ya kutoa mkono wa  pole nyumbani kwa  Rais wa awamu ya Pili ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi nyumbani kwao Migombani Zanzibar mjini leo Septemba 3, 2016

Friday, September 2, 2016

WAFICHA FEDHA ITAKULA KWAO..!!



Wakati wadau mbalimbali wa masuala ya Uchumi nchini Tanzania wakitoa maoni yao juu ya FEDHA ZILIZOFICHWA NA HATMA YA UCHUMI WA TANZANIA naye Profesa wa Uchumi, Chuo Kikuu cha Mzumbe, Honest Ngowi akisema haamini kama fedha zilizofichwa ni nyingi kiasi cha kuteteresha mzunguko wa fedha nchini na kutaka zitizamwe sababu za fedha kutoonekana, Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria (OUT) mkoani Iringa, Dk Bukaza Chachage alisema kuficha fedha kwa nia ovu ni kosa kubwa kwa sababu huhatarisha uchumi.

By Fidelis Butahe, Mwananchi fbutahe@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. 

Baadhi ya wachumi nchini wametofautiana kuhusu kauli ya Rais John Magufuli kutishia kubadili fedha ili kuwadhibiti watu wenye tabia ya kuzificha, huku Gavana wa Benki Kuu Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndullu akisema kauli ya kiongozi mkuu huyo wa nchi inajitosheleza na hawezi kutoa tafsiri yoyote.

Wakati Profesa wa Uchumi, Chuo Kikuu cha Mzumbe, Honest Ngowi akisema haamini kama fedha zilizofichwa ni nyingi kiasi cha kuteteresha mzunguko wa fedha nchini na kutaka zitizamwe sababu za fedha kutoonekana, Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria (OUT) mkoani Iringa, Dk Bukaza Chachage alisema kuficha fedha kwa nia ovu ni kosa kubwa kwa sababu huhatarisha uchumi.

Katika maelezo yake, Profesa Ngowi alisema ili kubadili fedha ni lazima kuweka matangazo ili wale wenye fedha zinazotaka kuondoshwa katika mzunguko waweze kuzitoa na kubainisha kuwa moja ya sababu ya kuzibadili ni kuongezeka kwa fedha bandia.

“Ili kuwadhibiti watu wanaoficha fedha, suluhisho si kuchapisha au kubadili fedha. Binafsi siamini kama kuna watu wameshika mabilioni kiasi hicho,” alisema na kuongeza: “Hapa suala la kutazama ni sababu za fedha kufichwa au kutoonekana. Unajua Serikali hii imebana matumizi, ukusanyaji kodi kwa sasa umeimarika, safari zimepungua kwa kiasi kikubwa, sekta binafsi nazo zinakosa fedha kwa kuwa Serikali imeanzisha utaratibu mpya, kama vikao kutofanyia katika mahoteli.”

Katika hilo, Dk Chachage alisema: “Ukificha fedha ndani maana yake bidhaa zinakuwa na bei kubwa na mahitaji ya fedha pia yanaongezeka kwa kasi na suala la kupata fedha linakuwa ngumu. Benki zinakosa fedha, hata kukopa pia hushindikana. Hapo suluhisho ni kuwabana wahusika kuziachia ili kuwe na mzunguko wa fedha unaokidhi utashi wa watu wote. Hilo la kubadili huwa hatua ya mwisho.”

Alisema uwepo wa fedha bandia ni sababu kubwa kwa Serikali kubadili fedha na kusisitiza kuwa watu wengine huamua kuficha kwa sababu zinakuwa za wizi.

Hata hivyo, mwanazuoni wa uchumi, Profesa Samwel Wangwe aliishauri BoT kuzungumzia jambo hilo kwa sababu kufanyika kwake ni lazima ijadiliane na Wizara ya Fedha.

DC BAGAMOYO AWAONGOZA WANANCHI WAKE KUFANYA USAFI AKIWA ANAENDESHA GARI LA TAKA TAKA MWENYEWE

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga akiwa katika anaendesha gari la aina ya trekta kwa ajili ya kupakia takataka  wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 52 ya jeshi la wananachi Tanzanaia (JWTZ) ambapo aliwaongoza wananchi wa bagamoyo kwa kufanya usafi katika mitaa mbali mbali (PICHA NA VICTOR MASANGU)

Caption- Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga akiwa na baadhi ya askari mgambo wakiwa wanafanya usafi katika maadhimisho ya jeshi la wananci wa Tanzania (JWTZ) (PICHA NA VOCTOR MASANGU)
 

NA VICTOR MASANGU,BAGAMOYO

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani Majid Mwanga amekemea na kuvipiga marufuku  vitendo vya askari mgambo kuwa na tabia ya kujihusisha na upitishaji wa kuingiza  biashara za magendo   na badala yake amewataka kuhakikisha wanakuwa wazalendo na nchi yao  kwa lengo la kuweza kudumisha hali ya amani na  utulivu.

Kauli  hiyo imetolewa wakati alipokuwa akizungumza na askari mgambo pamoja na wananchi mara baada ya kumaliza kusherekea maadhimisho ya miaka 52 ya Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ)ambayo yalikwenda sambamab na zoezi la ufanyaji wa usafi katika mitaa mbali mbali ya Wilayani  Bagamoyo ambayo pia yaliwajumuisha  wafanyakazi wa ofisi ya mkuu wa Wilaya.

Mwanga alibainisha  kwamba askari wanatakiwa kuwafichua wale wote ambao wanajihusisha na biashara hizo,ambazo zimekuwa zikiingia nchini kinyemela kupitia fukwe za bahari ya hindi  kinyume na sheria na taratibu na kupelekea kuikosesha  serikali kukusanya  mapato kama inavyotakiwa kutokana na watu wachache kukwepa kulipa kodi.

“Mbona mnavusha wahamiaji haramu, mbona mnaingiza sukari a magendo,mbona mnashiriki kuvusha tairi za magendo na cha kushangaza hamtuambii lolote, kwa hiyo mimi ninachowaomba tabia hii sio nzuri na kitu kikubwa ni kushirikiana bega kwa began a jeshi la Polisi ii kuweza kuwafichua wale wote ambao wanafanya biashara hizo za magendo,”alisema Mwanga.

Mwanga alisema kwamba kwa sasa wataweka mikakati kabambe kwa ajili ya kuweza kufanya msako wa mara kwa mara katika fukwe za bahari, ili kuweza kuhakikisha kwamba wale ambao wanajihusiha na biashara hizo z amagendo wanakamatwa na wanachukuliwa hatua kali za kisheria ili iwe fundisho kwa wengine.

Katika hatua nyingine Mwanga alisema kwamba katika mkuhakikisha Wilaya ya Bagmoyo inakuwa na mazingira masafi muda wote wameweka faini ya kisi cha shilingi elfu hamsini kwa mtu yoyote atakayebainika anatupa taaka ovyo na kuongeza kuwa kuna program maalumu ambayo itazinduliwa na kushindanisha kata kwa usafi na washindi watapatiwa pikipiki kwa maafisa tarafa na watendaji.

Kwa upande wao baadhi ya askari mgambo  akiwemo Frank Mwaisame pamoja na Hamis Ramadhani  hawakusita kuelezea changamoto zinazowakabili katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku na kuiomba serikali kuwangalia kwa jicho la tatu katika suala zima la maslahi yao kwani wanafanya kwazi kwa kujitolea.

Nae Katibu Tawala wa Wilaya ya Bagamoyo  Erica Yegella mewaasa wakinamama wanatumia fursa zilizopo kwa ajili ya kuweza kuleta chachu ya maendeleo pamoja na kuwaasa kufanya usafi katika maeneo yao ili kuepukana na magonjwa ya  mlipuko.

Reha Mita ni  Kaimu mshauri wa mgambo Wilaya ya Bagamoyo pamoja na  Mkuu wa jeshi la polisi Wilaya ya Bagagamoyo  Adam Maro ambaye ni mkuu wa jeshi la Polisi Wilaya ya Bagamoyo walisema askari wanapaswa kuwa wazalendo na nchi yao ili kudumusha amani iliyopo. na hapa walikuwa na haya ya kusema kuhusiana na maadhimisho hayo.

KATIKA kusherekea maadhimisho hayo ya miaka 52 ya Jeshi la wananzhi wa Tanzania (JWTZ)  Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo ameongoza zoezi la kufanya usafi kwa kuamaua kuendesha mwenyewe gari la kubebea  takataka  na kupita katika mitaa mbali mbali jambo ambalo liliweza kuwa ni kivutia kikubwa kwa wananachi.

NEW GENERATION ZANZIBAR, MBASPO MBEYA MABINGWA Airtel Rising Stars.

Nahodha wa timu ya New Generation Amina Hali Abdallah (nyekundu) akikabidhiwa kombe na Afisa Habari wa ZFA Ali Bakari baada ya kuichapa timu ya Women Fighter 2-1 kwenye fainali za michuano ya Airtel Rising Stars Zanzibar Jana 25 Agosti 2016. New Generation ilishinda 2-1.
Wachezaji wa timu ya New Generation wakishangilia baada ya kukabidhiwa kombe la ubingwa baada ya kuifunga Women Fighter 2-1 kwenye fainali za michuano ya Airtel Rising Stars Zanzibar, zilizochezwa kwenye uwanja wa Fuoni Alhamisi 25 Agosti 2016

Naodha wa timu ya Mbaspo Academy Mbeya, Biva Steven akipokea kikombe kutoka kwa mgeni rasmi Katibu Tawala wa mkoa huo Alone Mbinga baada ya timu yake kuifunga Uyole Alois Academy Penati 4-3  katika mchezo wa fainali ya Airtel Rising stars ngazi ya mkoa uli0pigwa katika dimba la uwanja Sokoine juzi.
Wachezaji wa Mbaspo wakishangilia baada ya kukabidhiwa kikombe cha ubingwa wa Airtel Rising Stars mkoa wa Mbeya juzi. 

New Generation, Mbaspo mabingwa Airtel Rising Stars
TIMU ya wasichana ya New Generation imefanikiwa kutwaa ubingwa wa michuano ya Airtel Rising Star, Zanzibar, baada ya kuifunga Women Fighter kwa mabao 2-1 katika fainali iliyochezwa visiwani humo jana.
Mchezo huo wa fainali uliopigwa katika uwanja wa Fuoni nje kidogo ya mji wa Zanzibar na kuvuta hisia za mashibiki wengi wa soka wanawake na wanaume, hasa kwa vile timu hizo zina upinzani wa jadi.
Mabao ya New Generation yote yalifungwa katika kipindi cha kwanza ambapo bao la kwanza lilifungwa na Warda Mwinyi katika dakika ya 10 wakati bao la pili lilifungwa mnamo dakika ya 16 wakati bao la kufutia machozi la Women Fighter lilifungwa na Khadija Hassan dakika ya 27.
Akizungumza wakati wa kukabidhi kombe kwa washindi afisa habari wa chama cha soka Zanzibar ZFA Ali Bakari Cheupe kwa niaba ya rais wa chama hicho, aliipongeza kampuni ya Airtel kwa uamuzi wake wa kudhamini michuano hiyo ambayo imeweza kuleta hamasa kubwa kwa wananchi wa Zanzibar.
Alisema kabla ya michuano hiyo Zanzibar ilikuwa nyuma katika soka la wanawake lakini kupata udhamini huo ari imeongezeka zaidi na tayari wanawake wengi wamehamasika kutaka kucheza mpira wa miguu.
Naye Meneja Mauzo wa Airtel Muhidin Mikidad alisema kuwa kampuni yake itaendelea kusaidia michezo hiyo kadri ya hali itavyokuwa, ambapo amewapongeza wananchi wa Zanzibar kwa kuwaunga mkono

Jijini Mbeya, timu ya wavulana ya Mbaspo Academy  imefanikiwa kutwaa ubingwa wa mashindano hayo ya kuibua vipaji vya wachezaji chipukizi baada ya baada ya kuifunga Uyole Alliance 4-3 kwa changamoto ya mikwaju ya penati.

Mchezo huo uliamuliwa kwa penati kufuatia timu hizo kutoka sare ya kufungana 3-3 katika muda wa kawaida wa dakika 90.

Katika mchezo huo ulipigwa juzi katika dimba la kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya ulishuhudia vijana wa Uyole Alliance kutoka nje kidogo ya jiji la Mbeya wakijipatia goli la kuongoza katika dakika ya saba baada ya Daniel Shaban kufunga kwa penati baada mchezaji wa timu hiyo kufanyiwa madhambi katika eneo la hatari.

Mbaspo walikuja juu na kufanikiwa kusawazisha katika dakika ya 20 kupitia kwa Albinus Haule kabla ya Claud Alex wa Uyole Alliance kuandika bao la pili timu yake dakika ya 42.

Mabao mengine kwenye mchezo huo yalipatikana dakika 82 kwa upande wa Mbaspo mfungaji Shadraki Sape,wakati bao la Uyole Alliance lilipatikana dakika ya 88 mfungaji ni Claud Casto.

TPSF YATOA MAFUNZO KWA WAJASILIAMALI MKOANI GEITA.

Katibu Tawala wa wilaya ya Geita Thomas Dimme akifungua semina ya wajasiriamali ya taasisi ya Tanzania Private Sector Foundation iliyofanyika wilayani humo
Mkuu wa kitengo cha wajasiriamali kutoka kutoka mfuko wa kuendeleza sekta ya fedha (FSDT) akiongea wakati wa mafunzo hayo.
Afisa Mwandamizi kutoka ofisi ya RAS ya Geita akiongea wakati wa mafunzo hayo.
Ni meneja Mradi wa mafunzo kutoka TPSF, Celestine Mkama,akitoa maelekezo kwa wanasemina
Baadhi ya wajasiriamali waliohudhuria mafunzo mafunzo hayo wakifuatilia mada mbalimbali kutoka kwa wakufunzi. --- TPSF yatoa wafunzo kwa wajasiriamali mkoani Geita. 

 Wajasiriamali waliopo mkoani Geita wametakiwa kutumia raslimali mbalimbali zilizopo mkoani humo na firsa zinazojitokeza kwa sasa kuibua miradi ya biashara na kuendesha biashara yao kitaalamu wakiwa na malengo ya kujikwamua kutoka katika hali ya umaskini. 

 Ushauri huo umetolewa na Katibu Tawala wa wilaya ya Geita,Bw.Thomas Dimme aliyemwakilisha Mkuu wa wilaya hiyo kama mgeni rasmi wakati wa mafunzo maalumu ya mbinu za kuendeleza wajasiriamali yaliyoandaliwa na taasisi ya Tanzania Private Sector Foundation. Bw.Dimme alisema kuwa serikali imefungua milango ya kuwasaidia wafanyabiashara wadogo kwa kutumia fursa zilizopo hivyo aliwataka kuibua miradi ya biashara na kuwa na utayari wa kukabiliana na changamoto mbalimbali zilizopo katika biashara kwa kipindi hiki mojawapo ikiwa ni ushindani mkubwa na kufanya biashara kwa kufuata njia halali zinazotakiwa ikiwemo kulipa kodi za serikali kwa mujibu wa sheria.

 Aliipongeza taasisi ya TPSF kwa kuendesha miradi ya mafunzo kwa wajasiariamali sehemu mbalimbali nchini “Nawapongeza kwa kuwafikishia mafunzo wajasiriamali wa ngazi za chini katika ngazi ya mikoa na wilaya kwa kuwa wafanyabiashara wakipata mafunzo kama haya kwa vyovyote wataweza kupata mafanikio katika shughuli zao”.Alisema Dimme. 

 Kwa upande wake Meneja Mradi wa Mafunzo kutoka taasisi ya TPSF,Celestine Mkama alisema kuwa taasisi hiyo inaendesha mradi wa kuwapatia mafunzo wajasiriamali kuhusiana na mbinu mbalimbali za kufanya biashara kwa lengo la kupata mafanikio.

 “Mafunzo haya yamelenga kuwapatia maarifa wafanyabiashara wadogo ili yawajengee uwezo wa kukabiliana na changamoto zilizopo katika biashara “Tafiti nyingi zinaonyesha kuwa wafanyabiashara wengi wadogo wamekuwa wakikosa mbinu za kufanya biashara kutokana na kukosa elimu ya biashara ndio maana tumeona tuwasaidie katika eneo hili la kuwajengea uwezo kupitia kuwapatia elimu ya ujasiriamali”.Alisema Bw.Mkama. 

 Mkama alisema baadhi ya masuala yanayofundishwa kupitia mafunzo haya ni utunzaji wa mahesabu ya biashara, nidhamu katika matumizi ya fedha,utunzaji wa kumbukumbu za biashara na jinsi ya kupanga miradi. Akiongea kwa niaba ya wajasiriamali wenzake,Bi.Elizabeth Bigambo ,aliishukuru taasisi ya TPSF kwa kuwafikishia elimu ya ujasiriamali. 

“Tuna imani mafunzo haya tuliyoyapata yatatusaidia katika kukuza biashara zetu na kukua kibiashara na kuchangia pato la taifa kwa njia ya kodi”.Alisema Bigambo.

Thursday, September 1, 2016

CHRISTIAN BELLA & ERIC OMONDI KUPAMBA SHINDANO LA KUMSAKA 'OZONA MISS LAKE ZONE MWANZA'

Warembo wanaoshiriki kinyang'anyiro cha shindano la Ozona Miss Lake Zone kwa Mwaka 2016 tayari wako kambini kwaajili ya fainali itakayopigwa tarehe 10 September 2016 katika ukumbi wa Rock City Mall Mwanza, sambamba na kupewa mafunzo mbalimbali na elimu pia wanajihusisha na shughuli mbalimbali za kijamii ikiwa ni pamoja na kutembelea vituo mbalimbali vya afya mkoa wa Mwanza na kutoa misaada hasa kwa akinamama na watoto.
BOFYA PLAY KUJUA MPANGO MZIMA.
Ni ndani ya mazoezi kinyang'anyiro cha kumsaka Miss Lake Zone 2016 warembo katika pozi.
Mapozi na style.
Ndiyo sisi.
We love you.
Bidhaa ndani ya moja wa wadhamini wa kinyang'anyiro hicho ambao ni TSN Shopping Mall.
Ze poz kwa Lake Zone Tents & Supplies.
Sanjari na kuzawadia nao pia huzawadiwa na hapa kila mrembo alizawadiwa na duka la Flora Beauty Shop.
Techno.
Impression Limited.
Mpango mzima uko hivi.

WANAFUNZI HEWA 639 WABAINIKA

Wilaya ya Arumeru yabaini uwepo wa wanafunzi hewa 639 katika shule msingi na sekondari zilizopo katika wilaya hiyo.

FR

LIVE KUPATWA KWA JUA NCHINI TANZANIA

11:33 Zaidi ya nusu ya jua imekwishafunikwa, kaubaridi kameanza. 

11:03 Takribani theluthi moja ya jua imefunikwa na  mwezi 9:48AM Watu waambiwa wajikusanye katika makundi yenye watu 30 ili wapewe vifaa vya kutazama kupatwa kwa jua 9:30am Mkuu wa wilaya Mbarali Rueben anawasili kwenye tukio na ulinzi usalama waimarishwa 9:21am  Umati wa watu wamiminika Rujewa, Mbarali kushuhudia kupatwa kwa jua kipete

11:03 Takribani theluthi moja ya jua imefunikwa  na mwezi

9:48AM Watu waambiwa wajikusanye katika makundi yenye watu 30 ili wapewe vifaa vya kutazama kupatwa kwa jua

9:30am Mkuu wa wilaya Mbarali Rueben anawasili kwenye tukio na ulinzi usalama waimarishwa

9:21am  Umati wa watu wamiminika Rujewa, Mbarali kushuhudia kupatwa kwa jua kipete

Viongozi wa serikali,  wanahabari wa ndani na nje ya nchi na wananchi wameshawasili katika eneo linalotumika kushuhudia kupatwa kwa jua.

Eneo hili lililopo Rujewa, Mbarali ambalo hutumika zaidi katika kuchimba mawe na kupasua kokoto leo limefurika watu ambao wapo hapo si kwa ajili ya kununua bidhaa hiyo ya ujenzi bali kusubiri kushuhudia tukio hilo la aina yake duniani.

Walimu wakiongozana na wanafunzi wa shule kutoka Mkoa wa Mbeya na jirani wamewasili hapa kama sehemu ya kuwafundisha wanafunzi kivitendo.

Askari wanarandaranda kila kona kuhakikisha usalama unaimarishwa.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makala aliyewasili pia katika eneo hili, amesema tukio hilo limefungua fursa kwa kila mtu Mbeya hasa Mbarali.

Amevishukuru vyombo vya habari kwa kuutangaza mkoa  na amewaambia wananchi wajikusanye katika makundi ya watu 30 ili wapewe vifaa vya kutazama kupatwa kwa Jua Tanzania.

Makalla amewataka wananchi kuwa makini kuangalia tukio hilo akisisitiza "Huu siyo mwisho wa dunia."

Waendesha bodaboda na bajaji wanaendelea kuwaleta watu hapa Rujewa kushuhudia kupatwa kwa jua.

Wednesday, August 31, 2016

MAHAKAMA YA BARAZA LA ARDHI NA NYUMBA YAREJESHA JENGO LA CCM KATA YA KIRUMBA KUTOKA KWA MWEKEZAJI

Na Peter Fabian, MWANZA.
 
AGIZO la Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Taifa, Rais Dk John Magufuli kwa viongozi na wanachama wa Chama hicho kuweka wazi mali za Chama ngazi za matawi, Kata, Wilaya na Mkoa pamoja na kutolewa taarifa ya mapato na matumizi yake kwa wanachama imeanza kuzaa matunda na kuwa chungu kwa wawekezaji na wapangaji kwenye majengo yake.

Hatua hiyo imepelekea Mahakama ya Baraza la Ardhi na Nyumba  Mkoa wa Mwanza  kumuamru mwekezaji wa aliyekuwa mpangaji wa jengo la biashara la Kirumba Resort linalomilikiwa na CCM Kata ya Kirumba katika Wilaya ya Ilemela, Benson Temba kuondolewa baada ya kushindwa kulipa kodi ya pango katika jengo hilo kinyume cha mkataba.
 
Uamuzi wa Mahakama hiyo unatokana na kesi namba 176 ya mwaka 2013  iliyofunguliwa na Bodi ya wadhamini wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM wa kata hiyo Abubakar Kweyamba dhidi ya mwekezaji huyo  akidaiwa kuingia mkataba tata na kushindwa kulipa kodi ya pango kama ilivyo kwenye mkataba wa upangaji wa jengo hilo.
 
Mlalamikiwa Temba  katika utetezi wake alidai kuwa aliingia makubaliano na wamiliki wa jengo kufanya ukarabati kwa shilingi milioni 60 na akaomba baraza hilo kutupilia mbali shauri hilo dhidi yake hoja na ambayo ilikataliwa na baraza.Awali alifungua shauri namba 36 la 2016 akipinga kuondolewa kwenye jengo.
 
Akisoma hukumu hiyo juzi kwa muda wa saa moja  (Agosti 26, 2016) Mwenyekiti wa baraza hilo, James Sillas alisema kuwa shauri hilo lilikuwa gumu kutokana na mvutano wa kisheria uliokuwepo baina ya mawakili wa wadai na mdaiwa ambapo alidai kuwa mdaiwa (Temba) alivunja mkataba kwa kulipa kodi ya pango kidogo kidogo kwa miezi mitatu  kinyume cha kifungu cha 3 (b) cha mkataba.
 
Sillas alieleza kuwa baraza hilo kwa kuzingatia ushahidi uliotolewa na mashahidi wa pande zote mbili na kwa kuzingatia maoni ya wazee wa baraza na sheria namba 2 ya baraza hilo ,maoni yao yalifanana kuwa mdaiwa alivunja mkataba na bazara hilo liligundua kuwa hakuwa tena na uwezo wa kifedha.
 
Sillas aliendelea kueleza kuwa baraza liligundua  kuingiwa kwa mkataba wa giza wa miaka mitano huku kukiwa na mwingine wa mwaka mmoja, na hivyo baraza kujiuliza kulikuwa na nini wakati fedha hazijalipwa za mkataba wa awali.
 
“ Kipengele cha 3( b) kinachomtaka mdaiwa (Temba) kulipa kodi ya pango kwa miezi mitatu mfululizo kiasi cha shilingi milioni 1,000,000 kila mwezi badala yake alikuwa akilipa kidogo kidogo, hivyo  kipengele hicho kilimyima uhalali wa kuendelea kuwa mpangaji,” alisema mwenyekiti huyo kwenye hukumu hiyo.
 
Kwamba hakuna ubishi kuwa kodi ililipwa Novemba 2015 lakini Desemba 2015 hadi Februari 2016 kodi haikulipwa na wadai kushindwa kuvumilia na hivyo wakaamua kufunga jengo ambalo tayari lilionekana kuchakaa.
 
Sillas alieleza kuwa baraza hilo limeridhika bila shaka,bila giza na wasiwasi  kwamba kulikuwa na mkataba wa kinyemela na kuamuru Temba kuondolewa kwenye jengo hilo na kukabidhiwa mali zake,pia azuiwe kufika kwenye jengo hilo baada ya kukabidhiwa mali zake aondoke huku Mahakama hiyo ikimuondolea gharama za kesi  na kudai kuwa mtu ambaye hajaridhika na uamuzi huo  rufaa iko wazi.
.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kirumba Abubakar Kweyamba akizungumza na waandishi baada ya uamuzi huo kutolewa na Mwenyekiti Sillas alisema kuwa wameridhika na uamuzi huo kwani mahakama imetenda haki na kumpongeza baraza hilo (Sillas) kwani shauri hilo lilichukua muda mrefu kumalizika kutokana na nguvu aliyokuwa nayo mdaiwa na mabishano ya kisheria kwa mawakili wa pande mbili.
 
Kweyamba alidai kuwa kesi hiyo ni ya nne kufunguliwa kwenye baraza hilo na mwenyekiti aliyesikiliza kwa mara ya nne alilazimika kufanya kazi hata nje ya muda kutokana  mawakili wa mdai kuweka visingio vya kuwa na kesi kwenye mahakama zingine.
 
“Tulikuwa tukihujumiwa na viongozi wetu wa juu Benard Ndutta (Wilaya na Mkoa) waliopita katika kusimamia shauri hili wakishirikiana na mwekezaji.Wakati kesi ikiendelea, lakini tumpongeze Katibu wa CCM Mkoa Miraji Mtaturu (DC wa Ikungi Singida) na Katibu wa CCM Wilaya ya Ilemela, Acheni Maulid kwa ushirikiano wao hadi leo uamuzi umetolewa na huu uwe mfano kwa viongozi wengine,”alisema.
 
Wito wangu kwa wanachama kushirikiana na viongozi kuwa watulivu wakati huu na waepuke kusikiliza baadhi ya wanachama na watu ambao wamekuwa wakijitokeza kutumia fursa za kuwachonganisha na kuwagawa kwa masilahi yao binafsi hivyo wawakatae na kujipanga kukitumikia chama ili kufikia malengo ya utekelezaji wa ilani ya CCM ya 2015/2020.