ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 11, 2016

MAKEKE YA MWINYI KAZIMOTO YAIPAISHA TENA SIMBA KWENYE KILELE CHA LIGI KUU.

Angalia jinsi mchezaji Mwinyi kazimoto akionyesha ukomavu wake katika soka wakati wa mechi iliyochezwa kati ya Simba na Ndanda FC.

WAKALA WA MAJENGO TANZANIA YAIPA MKATABA YONO AUCTION MART WA KUKUSANYA MADENI NCHINI

 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ,  Arch. Elius Mwakalinga (kushoto), akikabidhiana hati ya mkataba na Mwakilishi wa Kampuni ya Udalali ya Yono Auction Mart & Co. Ltd, Scollastica Kevela Dar es Salaam leo asubuhi, baada ya kampuni hiyo kushinda zabuni ya kukusanya madeni ya TBA kuanzia leo.
 Taswira meza kuu katika mkutano huo.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) , Arch Elius Mwakalinga (katikati), akizungumza katika mkutano huo kabla ya kutiliana saini na kampuni ya Yono. Kushoto Ofisa wa Idara ya Manunuzi, Mariam Kazoba.
 Ofisa wa Idara ya Manunuzi wa TBA, Mariam Kazoba, akitoa ufafanuzi mbalimbali katika mkutano huo.
 Mwakilishi wa Kampuni ya Udalali ya Yono Auction Mart & Co. Ltd, Scollastica Kevela (kulia), akizungumza katika mkutano huo ambapo alisema Yono wamejipanga kuwafikia wadaiwa wote wa TBA.
 Mkataba akisainiwa kwa pande zote.
 Wanahabari wakiwa bize kuchukua taarifa hiyo.
Ofisa Habari wa TBA, Mirembe Dashina (kulia), akiteta jambo na mwenzake katika mkutano huo.


Na Dotto Mwaibale

WAKALA  wa Majengo Tanzania (TBA), umecharuka kwa kuingia mkataba na Kampuni ya Udalali ya Yono Auction Mart & Co. Ltd ili kusaidia kukusanya madeni ya wadaiwa sugu ambao walikopa nyumba.

Wakati huo huo mwakilishi wa kampuni hiyo ya udalali ya Yono Auction Mart & Co. Ltd, Scollastica Kevela ametoa siku tatu kwa wadaiwa wote wa TBA kuhakikisha wanalipa fedha hizo kabla ya kufikiwa na kampuni hiyo ambayo Jumatano ya Machi 16 mwaka huu itaanza rasmi kazi ya kuwaondoa katika nyumba za wakala huo watumishi wote wanaodaiwa kwa kufuata sheria kama inavyoelekeza.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo wakati wa kutiliana saini na kampuni hiyo ya udalali kwa ajili ya kukusanya fedha kutoka kwa wadeni wa wakala huo  Mtendaji Mkuu wa TBA ,  Elius Mwakalinga alisema wamefia hatua hiyo baada ya kuona wadaiwa wao ambao wengi wao ni kutoka sekta za serikali kushindwa kulipa fedha hizo.

"Tumeingia mkataba na Kampuni ya Yono Auction Mart baada ya kushinda zabuni ambayo tulitangaza Februari 23,2016 na sasa kazi yote ya ukusanyaji wa fedha hizo itafanywa na kampuni hiyo" alisema Mwakalinga.

Mwakalinga alisema fedha nyingi za wakala huo zipo mikononi mwa wadaiwa wao ambapo kwa mkoa wa Dar es Salaam na Dodoma ni shilingi.Bilioni 6 na kwa waliokopa ni sh.milioni 800 huku fedha zinazodaiwa kwa ajili ya kutoa ushauri mbalimbali wa ujenzi ni sh.bilioni 6.95.

Mwakilishi wa kampuni  ya Yono Auction Mart & Co. Ltd, Scollastica Kevela alisema wametoa siku tatu kwa wadaiwa wote kuhakikisha wanalipa fedha hizo vinginevyo watafikiwa na kampuni hiyo ambayo imepanga rasmi kupita kila nyumba inayodaiwa na kuwa kila muhusika atatakiwa kuilipa kampuni hiyo asilimia tano ya fedha anazodaiwa na TBA.

TAASISI YA DORIS MOLLEL KWA KUSHIRIKIANA NA CBA WASAIDIA HOSPITALI YA MWANANYAMALA.

 Meneja Mahusiano wa Benki ya CBA, Caroline Makatu (wa pili kushoto)  akikabidhi msaada wa vitanda na mashine kumsaidia mtoto anayezaliwa kabla ya muda, kwa Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala, Dk. Delilah Moshi, katika hafla fupi iliyofanyika hospitalini hapo, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Maafisa kutoka Benki ya CBA wakiwa katika picha ya pamoja wadau waliofanikisha msaada huo katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
TAASISI ya Doris Mollel Foundation (DMF) kwa kushirikiana na Benki ya  CBA wametoa msaada vitanda viwili na mashine tatu za kuwasaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati vyenye wa vitu vyenye thamani ya Sh.milioni  mbili  katika Hospitali ya  Rufaa ya Mwananyamala  jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jana Jijini Dar es Salaam  Mkurugenzi wa DMF,  Doris Mollel, alisema  kwa kutambua umuhimu kwa sababu wanawakumbuka  wanawake wanaojifungua kabla ya wakati na kutoa msaada huo ni kutaka  kuokoa uhai wa watoto hao .

“Kutambua thamani ya watoto njiti tumeona katika kuokoa uhai na kuweza kufikia malengo tumeona ..mashine za kuwasaidia kufikia malengo yao kama walivyo watoto wengine…taasisi itaendelea kutoa mchango kwa jamii,” alisema Doris.

Naye Meneja Mahusiano wa Benki ya CBA ,Caroline Makatu amesema  kuna changamoto nyingi  hospitali ikiwemo na uhaba wa vifaa kwa kutambua hilo wametoa msaada huo  ili kusaidia mama na mtoto.

Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Dk. Delilah Moshi amesema wanashukuru kwa msaada huo uliotolewa na taasisi hizo kwa kutambua uwepo wa wanawake na kuziwezesha hospitali.

Amesema kwa sasa shida kubwa iliyopo kwa sasa ni uhaba wa majengo kutokana na nafasi chache za kuhifadhia watoto njiti kwa sababu idadi ya watoto inaongezeka.

“Kutokana na kuwapo kwa mashine za kuhifadhia watoto njiti idadi ya vifo vya watoto hao imepungua hivyo naiomba serikali kuongeza madaktari wa watoto kwani hadi sasa wapo wawili tu,” amesema Mushi.

DK.KIGWANGALLA AFUNGA MOCHWARI YA HOSPITALI YA TUMBI, AIPA MASAA 72

Tazama MO tv, kuona tukio hilo hapa:
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla ametoa siku tatu kwa uongozi wa Hospitali y teule ya rufaa ya Mkoa wa Pwani-Tumbi kufunga chumba cha kuhifadhi maiti (Mochwari) baada ya kubaini matatizo mbalimbali baada ya kufanya ziara katika hospitali hiyo.

Katika ziara hiyo, Dk. Kigwangalla alibaini mambo mbalimbali kutoenda sawa ikiwemo suala la utendaji mbovu ambapo alitoa agizo la kumtaka Mkurugenzi wa Shirika la Elimu Kibaha wanaosimamia Hospitali hiyo kutoa maelezo ndani ya masaa 24 kama anafaa kubaki ama la!.

Aidha, Dk. Kigwangalla amebainisha kuwa, hali aliyoikuta katika chumba cha kuhifadhia maiti ni mbaya hivyo ilikuondoa matatizo amelazimika kuifunga kwa muda huo wa siku tatu ilikufanyia marekebisho kwa baadhi ya mambo ndani ya chumba hicho cha mochwari hospitalini hapo.

Awali vyombo vya habari vilitoa taarifa mbalimbali juu ya Mochwari hiyo ikiwemo badhi ya maiti kuhifadhiwa nje na kuatarisha afya za wananchi.
tumbi99Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla (katikati) akiwa na uongozi wa Hospitali hiyo akiwemo Mganga Mkuu wa Hospitali, Dk. Peter Datani (kulia) akitembelea katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Pwani-Tumbi wakati wa ziara hiyo mapema jana Machi 10.2016.
tumbi hjjhNaibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akikagua Mochwari ya Hospitali ya Rufaa ya Tumbi
tumbi uuNaibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akikagua Mochwari hiyo. Ambapo hadi sasa licha ya matatizo inayoikabili mochwari hiyo haina umeme na vifaa muhimu ikiwemo kipima cha kupimia joto kuharibika.
tumbi zazaatumbi mochwariNaibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiangalia kifaa maalum ndani ya Mochwari hiyo ambapo hata hivyo hakifanyi kazi.
tumbi jklNaibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akitoa agizo hilo kwa uongozi wa Hospitali hiyo pamoja na viongozi wa Serikali juu ya kuifunga Mochwari hiyo kwa siku tatu hadi hapo itakapofanyia ukarabati mambo mbalimbali yanayoikabili Mochwari hiyo.
tumbi hjjNaibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla alipowasilia kwenye Mochwari hiyo wakati wa ukaguzi huo katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Pwani-Tumbi, mapema jana Machi 10.2016. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog-Kibaha,Pwani).

SAUTI SOL WAACHIA MTWANGO MPYA "UNCONDITIONALLY BAE" WAKIMSHIRIKISHA ALIKIBA

BOFYA PLAY KUSIKILIZA.
East African music giants – the award winning acts: Sauti Sol (Kenya) and Alikiba (Tanzania) release the new single/video: UNCONDITIONALLY BAE. The song is poised to unite fans across East Africa and Africa at large, through dance and its strong message. The video has a surprise twist that will get fans excited. UNCONDITIONALLY BAE is a danceable love ballad. In the song Sauti Sol and Alikiba sing about the difficulty of finding love in the modern day world. 

Shot in Kenya’s beautiful North Coast of Mombasa at the English Point Marina, the official video of UNCONDITIONALLY BAE has been shot by the South African video director Justin Campos of Gorilla Films. UNCONDITIONALLY BAE has been written by Sauti Sol and Alikiba, and produced by Sauti Sol.

Sauti Sol said in a statement: “We are thrilled to release this song. Our fans have been waiting for it, even demanding it, and it's time to honour that. Africa, we hope you love our first collaboration with Alikiba as much as we do. Alikiba is a legend and we are honoured to work with him.”

Alikiba said in a statement: “From the first time I met Sauti Sol I knew I had to work with them. I admire their style and I found that they loved mine too. It was so much fun and seamless working on this project. My Bongo family and fans across Africa – we present this to you.”

UNCONDITIONALLY BAE YouTube: https://www.youtube.com/watch?v=pLs4Tex0U1U

Please find the song and artwork attached in your email. Feel free to share widely within all your networks.  

EDITOR’S NOTES

In February of 2016, Sauti Sol launched their third album: Live and Die in Afrika in Nairobi as part of their 2016 Live and Die in Afrika nationwide tour. Live and Die in Afrika was added in BBC Africa’s Top 10 tracks of 2015 and Okayafrica’s Top 15 Albums of 2015. They were also listed as Billboard Africa’s Most Promising Music Group, The Standard Newspaper’s 2016 Agenda Setters and DRUM Magazine East Africa's 2015 Movers and Shakers.

Alikiba is one of East Africa's most respected artistes, mainly because of his masterful skill in song writing and hit making. The singer is celebrated for hits like Lupela and Chekecha Cheketua. In 2015, he bagged six awards at the Kilimanjaro Awards for his mega hit: Mwana. He has in the past few months enjoyed successful tours across Africa and USA. He is also a WildAid Ambassador and is passionate about eradicating elephant poaching in Africa.

For more: #SautiSolAlikiba #UnconditionallyBae 

WATATU WAFA KWA KUFUNIKWA NA KIFUSI GEITA.


Watu watano wamepoteza  maisha na wengine watatu kujeruhiwa vibaya kwa kuvunjika viungo vyao baada ya kufukiwa na kifusi wakati wakichimba mawe yanayodhaniwa kuwa ni dhahabu.

Tukio hilo limetokea juzi saa 9:00 Alasiri, katika kata ya  Mgusu Wilayani Geita  ambapo watu  hao waliangukiwa na ukuta wa udongo waliokuwa wakiuchimba.

Pamoja na tukio hilo la kusikitisha wachimbaji hao wakatoa kilio chao kwa Serikali kuhusu maeneo ya kuchimba yaliyo salama ikiwa ni pamoja na kuwapa zana za kuchimbia na uokoaji.

Katibu tawala ya wilaya ya Geita Gaspar Kanyaiita aliyetembelea eneo hilo ameagiza Ofisi ya Madini kuwakamata wachimbaji wote wanaokiuka kanuni huku kaimu Afisa Madini Mkoa wa Geita akisema eneo hilo limefungwa tangu jana mpaka itapotangazwa utaratibu mwingine.

Thursday, March 10, 2016

RAIS MAGUFULI ASITISAHA MALIPO YA ZAIDI YA BILIONI 900 BENKI KUU.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya ziara Benki Kuu ya Tanzania (BOT), ambapo pamoja na mambo mengine ameiagiza Benki hiyo kusitisha mara moja ulipaji wa malimbikizo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya ziara Benki Kuu ya Tanzania (BOT), ambapo pamoja na mambo mengine ameiagiza Benki hiyo kusitisha mara moja ulipaji wa malimbikizo ya malipo ambayo tayari yalishaidhinishwa (Ex-Checker) na badala yake yarejeshwe Wizara ya fedha na Mipango kwa ajili ya kufanyiwa uhakiki.

Rais Magufuli wakati Benki Kuu ya Tanzania ilikuwa katika mchakato wa kufanya malipo ya shilingi Bilioni 925.6, ambazo Wizara ya Fedha ilitoa idhini ya kufanyika malipo. 


TAZAMA VIDEO YA SAKATA HILO BOT ILIYORUKA TBC1
 
Akizungumza na watendaji wakuu wa Benki Kuu ya Tanzania waliojumuisha Gavana, Naibu Magavana, Wakurugenzi na Mameneja, Rais Magufuli ametaka Wizara ya Fedha ifanye upya uhakiki wa malipo hayo, ili kubaini kama walengwa walioidhinishwa kulipwa wanastahili kulipwa ama vinginevyo.

Aidha, Dkt. Magufuli ameagiza Kitengo cha madeni ya nje ambacho awali kilikuwa chini ya Benki Kuu na baadaye kikahamishiwa Wizara ya Fedha, kirejeshwe Benki Kuu mara moja ili kuimarisha udhibiti wa ukopaji na ulipaji wa madeni.

Wakati huo huo, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amemuagiza Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prof. Beno Ndulu kupitia upya orodha ya wafanyakazi wa Benki hiyo, na kuwaondoa mara moja wale wote ambao hawana ulazima wa kuwa wafanyakazi katika benki hiyo.

CHADEMA DK. SLAA SIO LOLOTE SI CHOCHOTE NAFASI YAKE KUZIBWA NA MTU MAKINI.

Tumain Makene ambaye ni Afisa Habari wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo nchini CHADEMA AKITOA TAARIFA YA mikutano inayoendelea kufanyika jijini Mwanza.
Chadema Dk. Slaa sio lolote si chochote
Nafasi yake kuzibwa na mtu makini
CHAMA cha Demokrasia na maendeleo Chadema, kimesema kuwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willbrod Slaa, si lolote na si chochote ndani ya chama hicho na kwamba nafasi yake itazibwa na mtu makini zaidi yake. 

Chadema ambacho kimejichimbia mkoani Mwanza, kujadili mambo mbalimbali ikiwemo ya kumpata mrithi wa Dk. Slaa pamoja na kujiwekea mipango mahususi ya chama hicho katika kipindi cha mwaka 2016/2020.

Dk. Slaa alijiondoa Chadema na kutangaza kuachana na masuala ya kisiasa, baaada ya chama hicho kikuu cha upinzania kumteua aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowasa kugombea urais kupitia chama hicho na kuungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi Ukawa.

Hata hivyo, katika uchuguzi wa mwaka 2015 vyama hivyo vilionekana kuwa na nguvu kubwa, ikilinganishwa na kipindi cha nyuma mwamko wa Wananchi kwa vyama vya upinzani ulikuwa ni mdogo ikilinganishwa na hivi sasa.

Katika matokeo ya uchaguzi huo, aliyekuwa mgombea Urais wa ukawa, Edward Lowasa alipata kura milioni 6 huku Rais wa Sasa, Dk. John Magufuli alipata kura milioni 8, kura ambazo hazijawahi kufikiwa na mgombea urais wa upinzani nchini.

Wakijdiliana kutoka kushoto ni Mbunge wa CHADEMA viti maalummkoa wa Mwanza, Bi Suzan Masele akifuatiwa na Afisa Habari Bw. Tumaini Makene (katikati) na kulia ni Tungaraza Jugu ambaye ni Afisa Oparesheni Kanda ya Ziwa Victoria.
Akizungumza na waandishi wa habari, Ofisa habari wa Chadema, Tumaini Makene, alisema kuwa ndani ya chama hicho wapo viongozi makini, wachapa kazi na watu wenye weledi mkubwa wa kukiongoza chama hicho.

Alisema kuwa pengo la Dk. Slaa  bado halijaonekana mahala popote pale na kwamba wafuasi wa chadema na wanachama watarajie Katibu mkuu ambaye ni makini na mchapa kazi ndani ya saa 48 zilizobaki.
Makene alisema kuwa watu wengi  wameanza kuzungumza mambo mengi ambayo hayana msingi wowote ndani ya chama ikiwemo kwamba ndani ya Chadema hakuna mtumwenye sifa ya kurithi mikoba ya Dk. Slaa.
Ndani ya Chadema kuna watu makini ambao ni zaidi ya Slaa. DK willbrod Slaa, nashangaa watu wanaodai kwamba hakuna mtu wa kuirithi mikoba yake, hii ni taasisi nitashangaa kuona watu wanasema mambo kama hayo.
Pia Makene alisema kuwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, anatarajia kuwasilisha majina mawili aliyopendekeza kwenye Baraza kuu la chama hicho lenye zaidi ya wajumbe 400 ili kuchagua jina moja.
Mpaka sasa hakuna jina ambalo limeishafahamika litapelekwa baraza kuu, anaefahamu ni mwenyekiti mwenyewe Freeman Mbowe, kwa hiyo muda uliobaki tusubili tuone ni nani atakaechaguliwa.
Waandishi wa Habari kikazi zaidi.
Majina ya ukatibu yanayotajwa
Mpaka sasa kuna majina mbalimbali yanayotajwa kushika nafasi ya ukatibu wa chama hicho yakiwamo, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibari, Salum Mwalimu, Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni KUB, Tindu Lissu.
Majina mengine yanayotajwa ni aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani, Fredrick Sumaye, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Bara, John Mnyika na Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijini, John Heche.
Licha ya majina hayo kutajwa kila kukicha na baadhi ya Wananchi na viongozi mbalimbali wa kisiasa, chama hicho kinatarajiwa kutangaza Katibu Mkuu wa Chadema katika mkutano wa hadhara.
                                Ratiba ya Vikao
Juzi na jana ilikuwa ni vikao vya kamati kuu ya chama hicho taifa, kesho ni kikao cha Baraza Kuu, ambapo katika kikao hicho kitapokea mapendekezo ya majina mawili yatakayowasilishwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe.
Kikao kingine ni Machi 13, ambacho ni cha Kamati Kuu kitakachoketi kwa siku moja na kisha jioni kutafanyika mkutano wa hadhara katika uwanja wa Furahisha uliopo Wilaya ya Ilemela mjini hapa.
                                      Wananchi wazungumza
Baadhi ya Wananchi waliozungumza, wakisema kuwa wanategemea kuona Katibu Mkuu wa chama hicho ambaye ni makini na hodari wa kujenga hoja kwa mstakabili wa kukikuza chama hicho kilichoanzishwa mwaka 1992.
Walisema kuwa endapo Katibu huyo wa chama hicho atachaguliwa kwa kufuata misingi na sheria ya chama, matarajio yao ni kuona Chadema mpya ya miaka mitano ya 2016 na 2021 kwa ajili ya ukombozi wa watanzania.
Unajuwa Katibu Mkuu wa chama ndio kila kitu na kama Chadema watachagua mtu ambae sio makini, ujuwe sasa hata mipango yao ya kulikomboa taifa haitafanikiwa tunategemea kuona mtu makini, alisema Edward Nyoni ambaye ni mchambuzi wa masuala ya kisiasa.

ZAIDI YA WASICHANA 500 JIJINI MWANZA WAFAIDIKA NA MRADI WA UGAWAJI TAULO ZA USAFI KWA AJILI YA KUJIHIFADHI WAKATI WA HEDHI.

Kushoto ni Bi. Khadija Liganga Mkurugenzi wa taasisi ya kusaidia wanawake na maendeleo ya wasichana yenye makao makuu jijini Mwanza, DidaVitengeWear Foundation akihimiza jambo juu matumizi mazuri ya vifaa vya usafi kwa wasichana wa shule ya sekondari ya Bujora (hawapo pichani), Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum Vijana mkoa wa Mwanza, Bi. Maria Kangoye Ndila ambae aliungana katika mradi huo kuwasaidia mabinti walio shuleni.
Wasichana wa Shule ya Sekondari Luchelele wakiwa katika picha ya pamoja na wawezeshaji toka DidaVitengeWear Foundation mara baada ya kupokea taulo za usafi (Pedi) na Elimu ya Usafi wa mwili na uzazi chini ya mradi wa Binti Box unaotekelezwa katika shule za Sekondari na Msingi kanda ya Ziwa.
Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa DidaVitengeWear Foundation ambae pia ni Mratibu wa Mradi wa Binti Box akijadiliana jambo na Mbunge wa Viti Maalum Vijana mkoa wa Mwanza kupitia CCM, Mh. Maria Kangoye Ndila (Katikati) pamoja na Mbunge wa Viti Maalum Wanawake mkoa wa Mwanza Mh. Zawadi Kiteto (Kushoto), wakati wa utekelezaji wa mradi wa kugawa taulo za usafi kwa Mabinti wa Shule ya Msingi Igombe.
Mkufunzi wa Afya ya Uzazi ambae pia ni muuguzi msaidizi kutoka kituo cha Afya cha Makongoro akitoa elimu ya usafi wa mwili na kuepuka mimba za utoto kwa wanafunzi wa kike wa shule ya msingi Igombe chini ya mradi wa Binti Box ulioandaliwa na DidaVitengeWear Foundation kwa kushirikiana na wadau mbalimbali jijini Mwanza.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Igombe wakiwa katika picha ya pamoja huku wakiwa na nyuso za furaha baada ya kupewa vifaa vya usafi vitakavyowasaidia katika mzunguko wao wa kila mwezi na kuepuka magonjwa mbalimbali yanayotokana na kutumia vifaa visivyo salama.
Mabinti wa shule ya sekondari ya Bujora iliyopo Wilayani Magu mkoani Mwanza wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa taulo za usafi toka taasisi ya DidaVitengeWear Foundation. 
Zaidi ya wasichana 500 jijini Mwanza wafaidika na mradi wa ugawaji wa taulo za Usafi kwa ajili ya kujihifadhi wakati wa hedhi

Katika kusheherekea siku ya Wanawake Duniani Machi 08,2016, taasisi ya kusaidia wanawake na wasichana yenye makao makuu jijini Mwanza, DidaVitengeWear Foundation, Imefanikisha kugawa taulo za usafi zaidi ya 2,000 kwa wasichana zaidi ya 500 wa shule moja ya msingi na mbili za sekondari, shule hizo ni Shule ya msingi Igombe Shule ya Sekondari Bujora na Shule ya Sekondari Luchelele zote za Jijini Mwanza kupitia mradi wa kuwasaidia Mabinti kufikia malengo yao, ujulikanao kama ‘Binti Box’. 

Hatua hiyo pia imefikiwa kwa ushirikiano wa karibu baina ya taasisi hiyo pamoja na Mtandao wa Wanawake jijini Mwanza wa ‘Women Roundtable’, na Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Mh.Stanslaus Mabula, Mbunge Viti Maalum Wanawake Mkoani Mwanza Zawadi Kiteto na Mbunge wa Viti Maalum Vijana Mkoani Mwanza Mh.Maria Kangoye Ndila.

Binti Box ni mradi ulioanzishwa kwa lengo la kuwasaidia watoto wa kike waliopevuka kubaki shule na kuimarisha mahudhuria ya wasichana shuleni kwa kuwapatia vifaa vya usafi vitakavyowasaidia wakati wa siku zao za hedhi. Wasichana wengi hasa wa vijijini hukosa kwenda shule kwa siku 5 mpaka 7 kwa mwezi kwa sababu ya kukosa vifaa vya usafi wakati wa mzunguko wa hedhi, hivyo mradi huu kwa upande wa kanda ya ziwa ni mkombozi kwa mabinti wengi kuhudhuria shule na kuinua kiwango cha ufaulu katika masomo yao.

Akiongea wakati wa kugawa taulo hizo za usafi mashuleni, Bi. Khadija Liganga, Mratibu wa Mradi na Mkurugenzi wa DidaVitengeWear Foundation, alieleza kwamba, elimu ya wasichana ni jambo la msingi katika jitihada za kuleta maendeleo kwa nchi masikini kwa sababu mafaniko ya wanawake hasa katika elimu inamaanika kuwa na faida ya muda mrefu na huenda mbali Zaidi katika kuinua uchumi wa jamii na nchi.

“Kuna sababu nyingi zinazochangia kudumaa kwa ustawi wa elimu ya mtoto wa kike hasa wale wa vijijini, tatizo la ukosefu wa vifaa vya usafi kwa mabinti wakati wa hedhi kwa kila mwezi nayo imeibuka kuwa ni tatizo sugu linalofumbiwa macho na wadau wengi wa maendeleo katika nchi zinazoendelea na Tanzania ikiwemo. Wasichana hawa hujawa na uwoga na kuhofia kupoteza thamani yao na utu wao wawapo shuleni au mbele za watu na kuwafanya wasihudhurie darasani au kutokwenda shule na matokeo yake wengi huacha shule,” amesema Bi. Khadija Liganga  

Bi Khadija aliendelea kusema kwamba “Baada ya kutembelea baadhi ya shule zilizo pembezoni na miji tumegundua tatizo ni kubwa, tukapata uwelewa wa kutosha na tukaona ni vyema badala ya kuandaa makongamano ya wanawake wakati wa sherehe za Siku ya Wanawake Dunaini 2016, kwanini tusiguse eneo ambalo ndio chimbuko la ukandamizaji wa maendeleo ya Mwanamke, ambalo ni Elimu. Ndipo tukaja na huu mradi utakaokuwa endelevu wa ‘Binti Box’ kwa lengo la kutoa taulo za usafi kwa mabinti wa shule za msingi na sekondari pamoja na elimu ya usafi wakati wa siku za hedhi”

“Tungependa kuwashukuru watu wote pamoja na taasisi mbalimbali kwa mchango wa o wa maboksi ya taulo za usafi. Huu ni mwanzo tu, huku mipango ikiwa ni kuongeza uwezo wa mradi kuweza kutoa huduma hii kwa shule za sekondari na msingi katika mikoa yote ya Kanda ya Ziwa, tuko tayari kushirikiana na watu binafsi au taasisi yoyote katika kumkomboa mtoto wa kike” alisema Bi. Khadija Liganga

Lengo la Mradi wa Binti Box ni kuwapatia elimu ya uzazi,afya,kuwajengea uwezo wa kujiamini na kuwapatia taulo za usafi wasichana wa sekondari na shule za msingi waliopo katika umri wa kuvunja ungo katika mikoa ya Mwanza na Mara. Mradi unatekeleza mpango wa taifa kwa vitendo wa kuhakikisha watoto wa kike hawabaki nyuma bali wanapata fursa sawa na wenzao wa kiume na kuongeza ufaulu kwa watoto wa kike.