ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 16, 2016

WALIOMWEKA HAI MWENZAO KWENYE JENEZA WASHTAKIWA.

Theo Martins Jackson
Theo Martins Jackson.
CHANZO/BBC SWAHILI.

Mtu mweusi nchini Afrika Kusini ambaye alidaiwa kulazimishwa kuingia katika jeneza na wakulima wawili weupe kwa kupita katika shamba lao amesema kuwa anahofia maisha yake.
Victor Mlotshwa alikuwa akizungumza nje ya mahakama ya mji wa kaskazini mashariki wa Middelburg ambapo waliotaka kumshambulia waliwasilishwa katika mahakama.
Theo Martins Jackson and Willem Oosthuizen,
Theo Martins Jackson na Willem Oosthuizen.

''Nilidhani wataniua'',alisema.
Kanda ya video ya dakika 20 iliorekodi kisa hicho imekuwa ikisambaa katika mitandao ya kijamii nchini Afrika Kusini.
Mwandishi wa BBC Pumza Fihlani huko Middelburg anasema kuwa ndani ya mahakama hiyo ,washtakiwa hao ,Theo Martins Kackson na Willem Oosthuizen,walisimama wakiwa wameinamisha vichwa vyao chini huku waandishi wa habari na raia wakichukua picha zao.

Victor Mlotshwa
Victor Mlotshwa.
Wameshtakiwa kwa kumteka nyara na kumshambulia kwa lengo kumjeruhi vibaya.Hawajakubali ama kukana mashtaka hayo.
Wawili hao wanazuiliwa hadi tarehe 25 Januari huku waendesha mashtaka wakisema kwamba walihitaji muda zaidi kuchunguza ,ikiwemo kuthibitisha video hiyo.

Mamake Mloshwa alishindwa kujizuia wakati wa kusikizwa kwa kesi hiyoMamake bw Mlotshwa alijawa na hasira na kushindwa kujizuia wakati wa kusikizwa kwa kwesi hiyo.Nje ya mahakama kulikuwa na kelele za wafuasi wa vyama vikuu nchini humo huku #RacismMustFall ikisambazwa katika mitandao ya kijamii.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.